TAASISI ya Sanaa na Utamaduni ya Tanzania Music Foundations (TAMUFO)
imempongeza mlezi wake Ritta Kabati kutunukiwa udaktari wa heshima
kutoka Chuo Kikuu cha Afrika.
Kwa mujibu wa Rais wa Tamufo, Dk Donald Kisanga wanatoa shukrani za
pekee kwa mlezi wao huyo ambaye mchango wake katika maendeleo ya jamii
ikiwemo Tamufo ni wa kupigiwa mfano.
Kisanga alisema umahiri wa Dk Kabati umesababisha kuteuliwa kuwa
Mbunge wa Viti Maalum, hivyo wanatoa wito kwa jamii ya Tanzania
kuitumia ipasavyo heshima aliyoipata mwanamama huyo.
"Sisi Tamufo tunapongeza uteuzi wa Dk. Kabati kwani unaendana na
anayoyafanya katika jamii hususani sisi wasanii ambao tumejipanga
kukua na kuendeleza kazi zetu," alisema Dk Kisanga.
Aidha Dk Kisanga alisema kutokana na ushirikiano ulio bora kati ya
Tamufo na Dk Kabati, nyanja ya sanaa hapa nchini na Afrika Mashariki
kwa ujumla itapiga hatua zaidi ya ilivyo sasa.
Mahafali ya kutunukiwa tuzo hiyo ya Udaktari yalifanyika Juni 15
jijini Lusaka Zambia ambako mahafali yake yalipambwa na bendi mahiri
zilizokuwa zikiimba nyimbo mbalimbali ukiwemo wimbo wa Taifa la
Tanzania.
Ritta Kabati alipata tuzo hiyo kutokana na mchango wake katika jamii
ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa
Iringa.
Rais wa Tamufo, Dk Donald Kisanga akimpongeza Ritta Kabati baada ya kutunukiwa udaktari wa heshima na Chuo Kikuu cha Afrika.
Mbunge wa Viti Maalum wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Ritta Kabati akipongezwa na Katibu Mkuu wa Tamufo, Stella Joel.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...