Thadayo
Ringo (kulia)Mkuu wa Kitengo kinachoshughulikia maswala ya watumiaji
huduma na bidhaa za mawasiliano (TCRA) Rolf kibaja mtaalamu wa maudhui
TCRA .
Na.Vero Ignatus, Arusha.
Mamlaka
ya Mawasiliano nchini TCRA imezindua wiki ya huduma kwa mteja katika
chuo cha uhasibu Njiro ikiwa sehemu ya kuielimisha jamii kwa
kushirikiana na watoa huduma za simu za mkononi.
Thadayo
Ringo ni mkuu wa kitengo kinachoshughulikia maswala ya watumiaji huduma
na bidhaa za mawasiliano (TCRA) amesema dhima ya wiki ya utumishi wa
umma imesimama kuhakikisha jinsi gani Taasisi za Umma zinawezesha
vijana kujiajiri pamoja na kuangalia muingiliano wa uhamiaji kutoka
vijijini kwenda mjini
Amesema kuwa wanaangalia jinsi gani wanaweza kuikumbatia
Teknolojia katika kusaidia utekelezaji wa utoaji huduma jumuishi na
kuhakikisha kwamba wanajenga utamaduni wa utawala bora.
Amesema
katika kuzingatia hayo TCRA ilichagua mikoa 5 ambayo inaadhimisha siku
hiyo ambapo ni pamoja na Arusha,Mwanza Mbeya Dar es saalam, Dodoma
ambapo wapo kwaajili ya kufanya kampeni ya kusajili watu wanaotumia
huduma za simu za mkononi kwa kusajili line zao kwa kutumia alama za
vidole .
Ringo
ametaja changamoto kubwa wanayokutana nayo ni pamoja na watu wengi
kufikiria kwamba zoezi hilo linalengo la kuchuliwa alama za vidole,bali
wao wanahakiki taatifa kwa kutumia alama za vidole,ambapo wengi wanasita
kujidikisha.
Aidha
amesema katika kipindi chote hicho wananchi wanaalikwa kuwatembelea,na
wao wapo tayari kujibu maswali mbalimbali ambapo amesema kuwa tangia
zoezi hilo limeanza muamko ni mkubwa na amesisitiza kuwa kabla ya kufika
disemba watakuwa wameweza kukamilisha zoezi hilo kwa asilimia
kubwa.Picha na Vero Ignatus.
Wanafunzi
wa chuo cha uhasibu Njiro wakiwa kwenye foleni ya kuchukua namba ya
kitambulisho cha Taifa kwaajili ya kusajili laini kwa mfumo wa Biometric
ambapo zoezi hilo limefanyika siku mbili chuoni hapo na siku tatu
watakuwa katika soko la kilombero .Picha na Vero Ignatus.
Mmoja wa wafanyakazi kutoka NIDA akinsaidia mteja aliyefika kupatiwa huduma ya kitambulisho cha Taifa.Picha na Vero Ignatus.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...