Thadayo Ringo (kulia)Mkuu wa Kitengo kinachoshughulikia maswala ya watumiaji huduma na bidhaa za mawasiliano (TCRA) Rolf kibaja mtaalamu wa maudhui TCRA .


Na.Vero Ignatus, Arusha.
Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA imezindua wiki ya huduma kwa mteja katika chuo cha uhasibu Njiro ikiwa sehemu ya kuielimisha jamii kwa kushirikiana na watoa huduma za simu za mkononi.



Thadayo Ringo ni mkuu wa kitengo kinachoshughulikia maswala ya watumiaji huduma na bidhaa za mawasiliano (TCRA) amesema dhima ya wiki ya utumishi wa umma  imesimama kuhakikisha jinsi gani Taasisi za Umma zinawezesha vijana kujiajiri pamoja na kuangalia muingiliano  wa uhamiaji kutoka vijijini kwenda mjini 


 Amesema kuwa wanaangalia  jinsi gani wanaweza kuikumbatia Teknolojia katika kusaidia utekelezaji wa utoaji huduma jumuishi  na kuhakikisha kwamba wanajenga utamaduni wa utawala bora.

Amesema katika kuzingatia hayo TCRA ilichagua mikoa 5 ambayo inaadhimisha siku hiyo ambapo ni pamoja na Arusha,Mwanza Mbeya Dar es saalam, Dodoma  ambapo wapo kwaajili ya kufanya kampeni ya kusajili watu wanaotumia  huduma za simu za mkononi kwa kusajili line zao kwa kutumia alama za vidole .

Ringo ametaja changamoto kubwa wanayokutana nayo ni pamoja na watu wengi kufikiria kwamba zoezi hilo linalengo la kuchuliwa alama za vidole,bali wao wanahakiki taatifa kwa kutumia alama za vidole,ambapo wengi wanasita kujidikisha.

Aidha amesema katika kipindi chote hicho wananchi wanaalikwa kuwatembelea,na wao wapo tayari kujibu maswali mbalimbali ambapo amesema kuwa tangia zoezi hilo limeanza muamko ni mkubwa na amesisitiza kuwa kabla ya kufika disemba watakuwa wameweza kukamilisha zoezi hilo kwa asilimia kubwa.Picha na Vero Ignatus.

Wanafunzi wa chuo cha uhasibu Njiro wakiwa kwenye foleni ya kuchukua namba ya kitambulisho cha Taifa kwaajili ya kusajili laini kwa mfumo wa Biometric ambapo zoezi hilo limefanyika siku mbili chuoni hapo na siku tatu watakuwa katika soko la kilombero .Picha na Vero Ignatus
Mmoja wa Afisa kutoka NIDA Julieth Raymond,akimsaidia kuelewa.mmoja ya mteja aliyetembekea banda hilo kwaajili ya kupata kitambulisho cha Kitaifa katika chuo cha uhasibu kilichopo Njiro Arusha.Picha na Vero Ignatus..

Wanafunzi wa chuo cha uhasibu Njiro wakiwa kwenye foleni ya kuchukua namba ya kitambulisho cha Taifa kwaajili ya kusajili laini kwa mfumo wa Biometric ambapo zoezi hilo limefanyika siku mbili chuoni hapo na siku tatu watakuwa katika soko la kilombero .Picha na Vero Ignatus.
Mmoja wa wafanyakazi kutoka NIDA akinsaidia mteja aliyefika kupatiwa huduma ya kitambulisho cha Taifa.Picha na Vero Ignatus.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...