Mkuu
wa Huduma na bidhaa wa Tigo David Umoh (kushoto) akiwa na Mkuu wa Idara
ya masoko wa Dstv Baraka Shelukindo (kati kati) na Mtaalamu wa Huduma
za Intaneni wa Tigo Allen Salaita wakipongezana baada ya uzinduzi wa
ushirikiano kati ya kampuni ya Tigo na Dstv utakaowawezesha wateja wa
kampuni hizo kushuhudia michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vifurushi vya
gharama nafuu.
Wafanyakazi wa Tigo pamoja na Dstv wakifurahi pamoja muda mfupi baada ya uzinduzi wa ushirikiano kati ya kampuni ya hizo mbili utakaowawezesha wateja wao kushuhudia michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vifurushi vya gharama nafuu.
Mkuu wa Idara ya masoko wa Dstv Baraka Shelukindo (kati kati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya kampuni ya Tigo na Dstv utakaowawezesha wateja wa kampuni hizo kushuhudia michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vifurushi vya gharama nafuu. Kushoto ni Mkuu wa Huduma na bidhaa wa Tigo David Umoh na kulia ni Mtaalamu wa Huduma za Intaneni wa Tigo Allen Salaita.
Mkuu wa Huduma na bidhaa wa Tigo David Umoh (kati kati) akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ushirikiano kati ya kampuni ya Tigo na Dstv utakaowawezesha wateja wa kampuni hizo kushuhudia michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vifurushi vya gharama nafuu. Kulia ni Mkuu wa Idara ya masoko wa Dstv Baraka Shelukindo na kushoto ni Mtaalamu wa Huduma za Intateni wa Tigo Allen Salaita.
Wateja
wa Tigo na DStv sasa wataweza kufurahia mechi za Kombe la Mataifa ya
Afrika mubashara wakiwa sehemu yeyote na kwa muda wowote, baada ya
makampuni haya mawili kuzindua ushirikiano maalum na mahususi ya huduma
ya DStv itakayowapa wateja wake fursa ya kutazamaa mechi hizo kupitia
DStv Now mobile App kwa gharama nafuu.
Akizungumzia
na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ushirikiano huo, tMkuu wa
Bidhaa na Huduma wa Tigo, David Umoh alisema ushirikiano huo na DStv
unaendana sambamba na lengo la kampuni hiyo kukuza maisha ya kidijitali
kwa kila Mtanzania. .
“Tunayofuraha
ya kuzindua huduma hii maalum ya DStv Now itakayowapa wateja wetu wa
Tigo katika msimu huu wa michuano ya Afrika kupata fursa nzuri ya
kutazama mechi mtandaoni na kushuhudia timu yao pendwa ya Taifa Stars na
timu nyingine zinazoshiriki mashindano haya makubwa barani Afrika,”
alisema Umoh.
Aliongeza,
“Kupitia mtandao wetu bora wa 4G, tunaweza kuwahakikishia wateja wetu
wanaotumia DStv fursa ya uhakika ya kuunganishwa mubashara na bila
usumbufu wowote kuangalia Kombe la Mataifa ya Afrika, kutoka sehemu
yeyote na muda wowote kupitia DStv Now App katika vifaa walivyonavyo.
Hii ni fursa nzuri pia kwa wale wateja ambao kwa sababu mbalimbali
hawatakuwa na nafasi ya kutazama kupitia televisheni zao.”
Kwa
mujibu wa Umoh, Tigo inawapa wateja wake waliounganishwa na DStv nafasi
ya kuchagua vifurushi vitatu. Cha kwanza ni kifurushi cha GB 1.5 kwa
gharama ya TSH 2000 kwa masaa 24, cha pili ni cha GB 6 kwa gharama ya
TSH 7000 kwa siku 7, na kifurushi cha tatu ni ya GB 16 kwa TSH 20,000 tu
kwa siku 30.
Vifurushi hivi maalum na vya gharama nafuu kwa watumiaji wa DStv Now vinapatikana kupitia www.tigosports.co.tz, Tigo Pesa App, na menyu za *147*00# na *148*00#.
Kwa
upande wake, Mkuu wa Idara ya Masoko Multichoice Tanzania, Ronald
Baraka Shelukindo, alisema uzuri wa DStv Mobile app ni kwamba inaweza
ikafanya kazi katika vifaa aina nne bila nyongeza ya gharama yeyote.
“Hakutakuwa
na gharama ya ziada kutazama DStv kupitia vifaa mbali mbali, kwa sababu
gharama zote zinakuwa zimeshalipiwa katika kifurushi cha mwezi cha
DStv. Ili kuweza kuangalia mechi za AFCON, wateja wa DStv wanachohitaji
kufanya ni kupakua DStv App katika simu janja zao, kompyuta mpakato,
tablet au vifaa janja vingine,” alisema Shelukindo.
Uzuri
mwingine wa kipekee ambao mteja anaweza kuupata kupitia huduma hii ni
kuwa wateja wa DStv wanapewa uwezo wa kuunganisha hadi vifaa vinne
tofauti kwa wakati mmoja kutazama vipindi vya DStv wakati huo
televisheni nayo ikiwa nayo imeunganishwa na kuendelea kutumika
kuangalia vipindi.
Shelukindo aliongeza, “Kujiunga na DStv Now wateja wanatakiwa kutembelea now.dstv.com,
na kufuata maelekezo ya kuweka jina na neno siri. Baada ya kumaliza
hatua hiyo rahisi, watakuwa na uwezo wa kupakua na kuingia katika kifaa
janja yeyote na taarifa zao walizoweka na kuanza kutazama mubashara
vipindi.”
Shelukindo
aliongeza kuwa, mechi za AFCON zitakuwa zinaonyeshwa kupitia vifurushi
vyote vya DStv kuanzia kifurushi cha bei ya chini kabisa mpaka kifurushi
cha DStv Premium. “Wateja wa DStv katika vifurushi vyote watakuwa na
uwezo wa kufurahia mechi zote 52 ya mashindano haya maarufu ya mpira.
Ushirikiano wetu na Tigo umefanya maisha kuwa rahisi kwa sababu inatoa
fursa kwa yeyote kufurahia mechi hizi popote pale,” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...