KATIBU Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo amewataka Watanzania kuchangamkia ufadhili wa masomo unaotolewa na shirika hilo ili kutanua uwezo wa rasilimali watu katika nyanja mbalimbali.
Alitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki wakati wa kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kwa Mtanzania, Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) unaojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship .

Mtanzania huyo kutoka Chuo Kikuu Huria Tanzania atakwenda Japan na Canada kwa miezi minne kufanikisha utafiti wake juu ya menejimenti ya ufahamu wa data katika Tehama unavyoweza kusaidia mfumo wa kujifunza wa wanafunzi.
Doreen ameibuka mshindi kati ya watu 280 walioomba nafasi hiyo.
Profesa Malebo aliwataka watanzania kutumia nafasi mbalimbali zinazotangazwa kushindaniwa na taasisi yake kutafuta masomo na kwamba taasisi hiyo huchagua kwa haki kwa kuzingatia vigezo na ushindani uliopo.

Alisema kwa sasa watu wengi hawajitokezi kuomba nafasi hizo za ufadhili kupitia Unesco, na kuwataka waombe kwa kuwa nafasi hizo huenda yule anayestahili kwenda kutokana na vigezo vilivyopo ambavyo ni vya kishindani.
“Natoa wito kwa watanzania kutumia nafasi tunazopewa na Unesco kwani ni msaada mkubwa katika kuimarisha na kuboresha elimu na kuwezesha watanzania hasa vijana kupata elimu ya kusaidia kusogeza mbele maisha” alisema Profesa Malabo.

Naye mgeni rasmi katika hafla hiyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako ameishukuru serikali ya Japan kwa kuwezesha Unesco kutoa ufadhili huo muhimu kwa taifa hili.
Akimwakilisha Waziri Ndalichako, Naibu Makamu Mkuu  wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Prof Cuthbert Kimambo  alisema kwamba serikali ya Tanzania pamoja na kushukuru Japan kwa kumwezesha Mtanzania huyo, pia inaamini wale waliomaliza mafunzo yao watarejea nchini na kuyafanyia kazi yale waliojifunza na kuleta maendeleo.

Alisema pamoja na kuleta ufanisi katika ubadilishanaji wa maarifa kupitia mafunzo hayo ni matarajio ya serikali kwamba wanaopewa mafunzo hayo watahamisha elimu hiyo kwa wenzao na kulisogeza mbele zaidi gurudumu la maendeleo.

Mpango wa masomo wa kutanua uwezo wa utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) unaojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship ulianzishwa mwaka 2000 na aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Unesco Koichiro Matsura kwa kutafakari maono ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan wakati huo , Keizo Obuchi ambaye aliamini katika uwezo wa watu katika kuibadili na kuijenga dunia hivyo haja ya kujiongezea maarifa zaidi ili kuwepo na maendeleo.

Lengo la programu hiyo ni kuwezesha kuwa na uhakika katika utunzaji wa mazingira, kuleta mazungumzo ya kimataifa na kuendeleza suala la mawasiliano na teknolojia. Programu hii ni matokeo ya ushirikiano kati ya serikali ya Japan na UNESCO katika kuendeleza rasilimali watu kwa nchi zinazoendelea.
Programu hii ambayo ilianzishwa mwaka 2001, imeshawezesha watu 290 hasa vijana watafiti, ambapo 82 wametoka Afrika, kutanua uwezo wao katika nyanja wanazozifanyiakazi.

Miongoni mwa nchi ambazo zimeshanufaika ni Tanzania ambapo katika programu ya mwaka 2014 na 2015, Fatuma Ubwa na Juliana Samuel Kamaghe, walipata nafasi ya kujiimarisha katika sekta ya habari na teknolojia ya mawasiliano.
Doreen Richard Mushi ambaye amekuwa mshindi wa UNESCO/Keizo Obuchi Research Fellowships ya mwaka 2018 alikuwa anashindana na watu wengine 280 na ameshinda katika nyanya ya habari na tekniolojia ya mawasiliano (Tehama).

Tuzo hiyo itamwezesha Doreen Mushi kufanyakazi kwa miezi miwili na watafiti wa taasisi ya Learning Analytics Centre ya Chuo Kikuu cha Kyushu nchini Japan, na miezi mingine miwili na watafiti wa kitivo cha elimu, Chuo Kikuu cha British Columbia mjini Vancouver, Canada.
Katika vyuo vyote viwili  Doreen Richard Mushi, aliyezaliwa Agosti 27, 1983 atafanya utafiti kuhusu takwimu na uchambuzi utakaosaidia mifumo ya kusoma kwa wanafunzi.
 Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi.Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. 
 Bi. Doreen Richard Mushi kutoka Chuo Kikuu Huria (OUT) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship  akisalimia wageni waalikwa (hawapo pichani) katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kutoka kushoto ni Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos, Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo pamoja na Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo
 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati wa hafla ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi. Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos akitoa salamu za Unesco wakati wa hafla ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi. Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Bi. Doreen Richard Mushi kutoka Chuo Kikuu Huria (OUT) akizungumza jambo mara baada ya kutangazwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo akitoa neno la shukrani kwa wageni waalikwa (hawapo pichani) waliohudhuria hafla ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi. Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto akimpongeza Bi. Doreen Richard Mushi kutoka Chuo Kikuu Huria (OUT) kwa kushinda tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (katikati) akimpongeza Bi. Doreen Richard Mushi mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto na kulia ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo aliyemwakilisha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako.
 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo akimpongeza Bi. Doreen Richard Mushi mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo na kulia ni Naibu Katibu Mtendaji – Utawala na Fedha wa Tume ya Taifa ya UNESCO (NATCOM), Bw. Francis Msungu.
 Baadhi ya wageni waalikwa katika hafla fupi ya kutangazwa kwa mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti Bi.Doreen Richard Mushi kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo, Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos, Bi. Doreen Richard Mushi pamoja na mume wake, Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto pamoja na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo wakiwa katika picha pamoja mara baada ya tuhitimisha hafla ya kumtangaza mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja Kutoka kushoto ni Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco), Profesa Hamisi Malebo (kushoto), Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe.Shinichi Goto (wa pili kushoto),Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (wa pili kulia), pamoja na na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam-Utafiti (UDSM), Prof Cuthbert Kimambo (kulia) katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
 Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja na meza kuu pamoja na sekretarieti iliyoshiriki mchakato huo.
 Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa na maafisa wa Ubalozi wa Japan katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan jijini Dar es Salaam.
 Bi. Doreen Richard Mushi (katikati) mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wahadhiri wa vyuo vikuu mbalimbali nchini katika hafla fupi iliyofanyika nyumbani kwa Balozi wa Japan jijini Dar es Salaam.
Bi. Doreen Richard Mushi mshindi wa tuzo ya kwenda kujinoa zaidi katika utafiti kupitia Mpango wa Masomo wa Kutanua Uwezo wa Utafiti kwa udhamini wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) inayojulikana kama The Unesco/Keizo Obuchi Research Fellowship akiwa kwenye picha ya pamoja na Afisa kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Regina Monyemangene (kushoto).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...