Na, Editha Edward-Tabora 

Baadhi ya wazazi na walezi wa Mkoani Tabora  wanatuhumiwa kutumia vibaya sheria ya Elimu no, 25 Ya siku 90 zinazoweza kumfuta mtoto shule huku wengine wakitumia nafasi hiyo kuwaozesha watoto wakiwa na umri mdogo na wengine kutumikishwa katika shughuli za kiuchumi 

Ameyasema Hayo mkuu wa Wilaya John Mwaipopo katika kilele cha siku ya mtoto wa Afrika ambapo hufanyika kila ifikapa Tarehe16/6 kila mwaka 

Katika kuhakikisha mtoto anapata haki zake za msingi Shirika lisilo la Kiserikali la World Vision linalopambana na kutetea haki za mtoto ikiwa ni mimba na ndoa za utotoni, John Masenza Meneja wa Shirika la World Vision amesema kila mzazi au Mlezi analo jukumu la kulea Watoto na kuwatunza katika maeneo wanayoishi na Kushirikiana kwa pamoja na shirika hilo na kutoa taarifa za unyanyasaji wanaofanyiwa Watoto 

Akisoma risala kwa niaba ya Watoto wengine katika kilele hicho cha mtoto wa Afrika James Jackob amesema anapata faraja kubwa kuona Serikali ya Tanzania na Serikali za nchi za nje zimedhamilia kuimarisha harakati za kumkomboa na kumlinda  mtoto.
 Pichani ni Watoto waliowakilisha wanafunzi wote kutoka katika wilaya ya Igunga wakisoma Risala mbele ya mkuu wa Wilaya.
Wanafunzi kutoka Shule mbalimbali Wilaya Igunga wakiwa kwenye Maandamano ya kupinga Manyanyaso siku ya mtoto wa Afrika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...