Na Francis Godwin,  Iringa

Diwani kata ya Mwangata  jimbo la Iringa mjini Nguvu  Chengula alazimika kuwapigia magoti viongozi  na  wanachama  wa vikundi  vya wajasiliamali vya umoja wa wanawake Tanzania (UWT) kata ya Mwangata  kuwaomba  kutorudia  makosa ya usaliti waliyoyafanya  mwaka 2015  ya  kuchagua viongozi  wa upinzani na  kuomba sasa wachague viongozi wa   serikali za mitaa pia  madiwani ,wabunge na Rais Dkt John Magufuli mwaka 2020.

" Naomba  kuwaomba  sana  tena sana ninyi wanachama na viongozi wa UWT kata ya Mwangata tuepuke  usaliti wakati wa uchaguzi simamieni na waelimisheni wananchi  wachague viongozi  wanaotokana na CCM ili kuleta  heshima kwa chama ...kwanza naomba kuwapigia magoti kabisa maana  naomba  kutoka moyoni chagueni CCM "  alisema Chengula huku akiwa amepiga magoti 

 Diwani   huyo  aliyasema hayo alifikia uamuzi huo wa  kuwapigia magoti wanavikundi hao jana katika  ukumbi wa Damu ya Yesu wakati  wa  uzinduzi  wa   vikundi nane  vya ujasiliamali vya  umoja wa wanawake Tanzania (UWT) kata ya  Mwangata  . 

Alisema kuwa  sehemu  kubwa   vikundi ndani ya Manispaa ya  Iringa havijafikiwa na  mikopo  hiyo  kutokana na uamuzi  wa  wananchi walioufanya  mwaka  2015  kwa  kuchagua madiwani wa upinzani na mbunge wa upinzani  ambao wamekuwa  hawashughuliki na kero za  wananchi  zaidi ya  kujitazama  wao  hivyo   njia pekee ni kutorudia makosa kwenye  uchaguzi wa  serikali ya mitaa  na uchaguzi mkuu mwaka 2020 kuhakikisha  wanachagua  viongozi  watokanao na CCM pekee.

Aidha  aliitaka Halmashauri ya  Manispaa ya  Iringa  kutoa  mikopo  inayopaswa  kutolewa  kupitia makusanyo yake ya  ndani ya  kwa  vikundi  vya wajasiliamali wa kata ya Mwangata  ili  kuwawesha  kukuza  mitaji yao kwani  lengo  la  serikali  kuagiza  Halmashauri  kutoa mikopo  isiyo na  riba kwa wanawake ,vijana na  walemavu  ni  kuwawezesha  kupanua  wigo  zaidi ya shughuli zao .

Diwani   Chengula  alisema kwa  ajili ya  kuviwezesha  vikundi  hivyo  kusajiliwa katika Halmashauri  tayari  mbunge wa  viti maalum  mkoa wa Iringa Rose  Tweve ( CCM)  amevitembelea  vikundi  vya kata ya Mwangata  na kuvisaidia  fedha  kiasi cha shilingi 500,000 kwa  ajili ya  kukuza  mitaji huku  yeye kama  diwani wa kata  ameviongeza  kiasi cha shilingi 800,000 ili  kuviongezea  nguvu ya  kusajiliwa kisheria.

“ Serikali ya  chama cha mapinduzi (CCM) chini ya mwenyekiti  wetu Rais Dkt  John Magufuli  ipo  kuona  wananchi  wenye  sifa ya  kupewa  mikopo  hii wananufaika nayo na mikopo  hii haitakiwi  kurejeshwa kwa  riba yoyote  hivyo ni haki ya  kila mwenye sifa  kupewa mikopo  hiyo  iwapo atakuwepo  kwenye kikundi “  alisema Chengula.
Hivyo  alisema  fedha   hizo ni haki ya   makundi  husika na lazima Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa  kutoa mikopo  hiyo kwa makundi hayo  bila  kuwepo kwa ubaguzi  wowote  iwapo  vikundi  vitakuwa  vimetimiza sifa  zinazohitajika .
“ Mimi kama  diwani  wenu nitahakikisha napambana  kuubana  uongozi wa  halmashauri ya Manispaa ya  Iringa  ili  fedha  hizo  ziweze  kutolewa kwa  vikundi  vyote ambavyo  vitakuwa  vimetimiza   sifa  ya  kupewa  mikopo  hiyo na sitakubali  kuona  mnahangaika   kutafuta mitaji  wakati  fedha za  serikali zipo “  alisema Chengula
Kuwa  vikundi  vya kata  hiyo  vimekuwa mfano wa  vikundi  vingine   ndani ya Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa  kutokana na aina  ya  shughuli za uendeshaji wa  viwanda  vidogo vidogo  vya utengenezaji batiki na vikapu  vya  kisasa  ambavyo wanachama  wake  wamekuwa  wakifanya na shida  yao ni  mitaji ya  kuboreshea huduma  zao.
Naibu  meya  wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Joseph Ryata  alisema kuwa  uhakika wa  vikundi  hivyo kupewa mikopo upo  na kutaka kukamilisha taratibu za usajili wa  vikundi  hivyo  hasa  vile ambavyo havijasajiliwa .

Aidha  alisema  wajibu  wa halmashauri  hiyo kuendelea  kuwaunganisha  wananchi wake  na taasisi za  kifedha  zinazotoa mikopo nafuu kama inayotolewa na shirika la kuhudumia  viwanda  vidogo vidogo (SIDO) mkoa wa Iringa .
Awali  wanavikundi hao wakitoa changamoto  zao wakati wa kikao  hicho cha  uzinduzi wa vikundi vya   vya wajasiliamali kata ya Mwangata  walisema changamoto  kubwa ni Halmashauri  kushindwa  kutoa mikopo kwa  wakati .

 Diwani  wa kata ya Mwangata  katika Halmashauri ya manispaa ya  Iringa  Nguvu  Chengula akiwa amepiga magoti kuomba wanachama  wa  vikundi vya ujasiliamali  vya umoja wa wanawake Tanzania (UWT) kata ya Mwangata  kusaidia CCM kushinda kwenye  uchaguzi wa serikali za  mitaa jana  wakati wa  uzinduzi wa vikundi hivyo ukumbi wa damu ya Yesu Mwangata (Picha na Francis Godwin)
 Diwani  wa  kata ya  Mwangata  Nguvu  Chengulla  akionyesha  fedha  kabla ya  kuwakabidhi  wanavikundi kwa  ajili ya usajili wa  vikundi
Diwani  wa  kata ya  Mwangata  Nguvu  Chengulla  akikabidhi   fedha   wanavikundi kwa  ajili ya usajili wa  vikundi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...