Na Editha Karlo,Michuzi TV.
NAIBU
Waziri wa afya,maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Faustin
Ndugulile ameitaka sekta ya afya Mkoani Kigoma kutoa elimu kwa
watumishi wote wa afya kutambua hatua za kukabiliana na ugonjwa wa Ebola
Ndugulile
amesema kuwa endapo elimu itatolewa kwa wakati ikiwa ni sambamba na
kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama na kuwashirikisha wananchi
kikamilifu ugonjwa wa Ebola utathibitiwa kwakuwa kila mmoja atakuwa
anafahamu namna ya kuutambua ugonjwa huo.
"Elimu
ikitolewa kwa wakati kwa kuwashirikisha wananchi kikamilifu ugonjwa wa
Ebola tutaweza kuuthibiti kwani kila mtu anakuwa anaufahamu baada ya
kupata elimu"alisema
Pia
alisema kuwepo na uangalizi katika mipaka ili kuzuia watu kuingia
kutoka nchi za jirani na kuingia nchini kiholela.Mkuu wa Mkoa wa Kigoma
Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga amesema Mkoa wa Kigoma
unachangamoto ya mipaka,lakini hatua mbalimbali zinachukuliwa kuthibiti
wanaoingia kihohela nchini.
Naye
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt Paul Chaote amehaidi kuyafanyia kazi
maagizo ya Naibu Waziri ikiwemo la kutoa elimu ili kuthibiti ugonjwa wa
Ebola.
Naibu
waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia wazee na watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua bandari ya Kigoma ambapo wageni kutoka nchi za
jirani wanaitumia kuingia nchini
Naibu
Waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia wazee na watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua vituo vya dharula katika bandari ya Kibirizi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...