Na Editha Karlo,Michuzi TV.

NAIBU Waziri wa afya,maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Faustin Ndugulile ameitaka sekta ya afya Mkoani Kigoma kutoa elimu kwa watumishi wote wa afya kutambua hatua za kukabiliana na ugonjwa wa Ebola

Ndugulile amesema kuwa endapo elimu itatolewa kwa wakati ikiwa ni sambamba na kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama na kuwashirikisha wananchi kikamilifu ugonjwa wa Ebola utathibitiwa kwakuwa kila mmoja atakuwa anafahamu namna ya kuutambua ugonjwa huo.

"Elimu ikitolewa kwa wakati kwa kuwashirikisha wananchi kikamilifu ugonjwa wa Ebola tutaweza kuuthibiti kwani kila mtu anakuwa anaufahamu baada ya kupata elimu"alisema 

Pia alisema kuwepo na uangalizi katika mipaka ili kuzuia watu kuingia kutoka nchi za jirani na kuingia nchini kiholela.Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga amesema Mkoa wa Kigoma unachangamoto ya mipaka,lakini hatua mbalimbali zinachukuliwa kuthibiti wanaoingia kihohela nchini.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Dkt Paul Chaote amehaidi kuyafanyia kazi maagizo ya Naibu Waziri ikiwemo la kutoa elimu ili kuthibiti ugonjwa wa Ebola.
Naibu waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia wazee na watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua bandari ya Kigoma ambapo wageni kutoka nchi za jirani wanaitumia kuingia nchini
Naibu Waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia wazee na watoto Dkt Faustine Ndugulile akikagua vituo vya dharula katika bandari ya Kibirizi.
Naibu wa Waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia wazee na watoto Dkt Faustine Ndugulile akiongea na mkuu wa Mkoa wa Kigoma Brigedia Jenerali mstaafu Emanuel Maganga juu ya mikakati ya kuthibiti ugonjwa wa ebola usiingie Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...