Spika wa Bunge la Kenya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika, Mhe. Justin Muturi akiongoza kikao cha Kamati hiyo Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo. Wa kwanza Kulia ni Katibu wa CPA-Kanda ya Afrika na ambaye pia ni Katibu wa Bunge la Tanzania Ndg. Stephen Kagaigai na  wanaofuatia upande huo ni Wajumbe wa Sekretarieti ya Kamati hiyo  . Upande wa kushoto ni Wajumbe wa Kamati hiyo na ambao pia ni Wabunge kutoka Zambia, Uganda,Namibia, Ghana na Kenya.
 Spika wa Bunge la Kenya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Justin Muturi akiongoza kikao cha Kamati hiyo Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo.  Wakwanza kushoto ni Naibu Spika wa Bunge la Cameroon Mhe. Emilia Lifaka.  Pia, wanaofutia upande huo ni Wajumbe wa Kamati hiyo kutoka Bunge la Zambia, Uganda na Namibia.
  Katibu wa CPA-Kanda ya Afrika na ambaye pia ni Katibu wa Bunge la Tanzania Ndg. Stephen Kagaigai (wa kwanza kulia) akizungumza wakati wa kikao hicho.
 Spika wa Bunge la Kenya ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Justin Muturi akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge la Cameroon Mhe. Emilia Lifaka alipowasili kwa ajili ya kikao hicho. PICHA NA BUNGE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...