Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe akizungumza na Wakurungenzi wa Taasisi zilizopo chini ya ofisi hiyo walipokutana kujadili maeneo ya ushirikiano katika utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka wa fedha 2019 – 2020.
Mkurungenzi wa Idara ya Ajira na Ukuzaji Ujuzi Bw. Ally Msaki akielezea jambo kuhusu uwasilishwaji wa mpango kazi kwa kila taasisi wakati wa kikao kilichowakutanisha kujadili maeneo ya ushirikiano yanayoitaji utekelezaji wa pamoja.
Baadhi ya Wakurugenzi wakifuatilia kwa makini maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano jengo la PSSSF, Jijini Dodoma. Wa kwanza kulia ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba.
Sehemu ya wataalamu wa mipango na bajeti kutoka kwenye taasisi wakifuatilia maelezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe (hayupo pichani) wakati wa kikao hicho kilichofanyika, Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wakurugenzi wa Idara kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu wakisikiliza maelekezo ya Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe (hayupo pichani), wakati wa kikao kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Bw. William Urio akielezea jambo wakati wa kikao kilichowakutanisha kujadili maeneo ya ushirikiano yanayoitaji utekelezaji wa pamoja.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Afya na Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda akiwasilisha taarifa ya malengo mkakati na kazi zilizopangwa kutekelezwa na taasisi hiyo kwa mwaka 2019 – 2020.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe akipitia taarifa ya malengo mkakati na kazi zilizopangwa kutekelezwa na taasisi ya OSHA kwa mwaka 2019 – 2020, wakati wa kikao kilichowakutanisha kujadili na kukubaliana maeneo ya ushirikiano.
Mkurugenzi wa Mipango kutoka Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Bezil Ewala akiwasilisha taarifa ya malengo mkakati na kazi zilizopangwa kutekelezwa na taasisi hiyo kwa mwaka 2019 – 2020, wakati wa kikao hicho.PICHA ZOTE NA KITENGO CHA MAWASILIANO
OFISI YA WAZIRI MKUU (KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU)
………………

NA MWANDISHI WETU

Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) Bw. Andrew Massawe amekutana na Wakurugenzi wa Taasisi zilizopo chini ya ofisi hiyo kwa lengo la kujadili kwa kina maeneo watakayo shirikiana kwa pamoja katika mpango kazi wa mwaka 2019 – 2020 na kutoa maelekezo juu ya namna bora ya kuhudumia wananchi kulingana na huduma zinazotolewa na taasisi hizo.

Akizungumza wakati akifungua kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano uliopo jengo la PSSSF Jijini Dodoma, alisema kuwa Mwaka wa fedha 2019/2020 ni muhimu kukubaliana kwa pamoja maeneo ambayo yatatekelezwa kwa ushirikiano ili kuimarisha utendaji wa shughuli mbalimbali.

“Lengo kuu la kukutana kwetu hapa ni kuangalia utekelezaji wa shughuli zilizopangwa kwenye mpango kazi wa kila Taasisi katika mwaka huu wa fedha, na kubaini namna bora ya kutekeleza maeneo hayo kwa ufanisi,” alisema Massawe.

Katibu Mkuu aliongeza kuwa kupanga na kukubaliana maeneo ya ushirikiano katika utekelezaji wa mpango kazi kutasaidia kuongeza tija katika utendaji wa kazi na majukumu ya kila siku.“Ninapenda kuona tunakuwa mfano wa kuingwa kwa kujijengea mwenendo mzuri wa kushirikiana katika utendaji ili kufanikisha shughuli nyingi kwa wakati mmoja,” alisisitiza Massawe

Aidha, alitoa wito kwa wakuu hao kuzingatia suala la mawasiliano na uhusianao kwa wadau na wateja wanaowahudumia ikiwemo kufanyia kazi malalamiko yanayotolewa kwa wakati.

Kwa Upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Afya na Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda alieleza kuwa ushirikiano na taasisi nyingine na wizara ni fursa pekee itakayo wawezesha kutekeleza dhamira na mikakati waliyopanga ili kuleta maendeleo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bw. Masha Mshomba alisema kuwa yapo maeneo mengi ya kushirikiana kwa pamoja na mpango kazi wa mwaka ni sehemu ya utekelezaji wa maazimio yatakayo wasaidia kuwa na ushirikiano endelevu katika maeneo mbalimbali.

Kikao hicho kiliudhuriwa na Wakurugenzi na Wataalamu wa Mipango na Bajeti kutoka Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) na Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...