Na Hadija Seif
MSANII wa Muziki wa Injili nchini Irene Robert adondosha Mkwaju mpya kwa shabiki zake, ikiwa na bada ya kukamata anga la Muziki la Injili Tanzania na Nje ya Mipaka kwa wimbo wake uitwao "Kishindo".
Sasa ameshusha wimbo Mpya na video Uitwao Tembea, ambao ni wimbo wake wa nne kuachia baada ya kuachia "Unashuka", "Nianze na wewe", na sasa "Kishindo".
Irene ni mwimbaji ambaye amepata mafanikio kwa haraka sanaa kutokana na kufanya kazi nzuri za kiwango Cha juu sana.
Kazi ya video imefanywa na Enxer na audio ikifanyika pale Masai Record chini ya producer Yusuph Manamba akiwa chini ya Lebo ya Famara Promotion.
Ni mwimbaji aliyejishusha kwa Unyenyekevu na anatamani kwenda kimataifa zaidi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...