Afisa Mkuu wa Wateja Wadogo na wa Kati – filbert Mponzi (Kushoto) akikabidhi mfano wa Hundi kwa Mwenyekiti wa ALAT Taifa – Mh Gulamhafeez Mukadam ikiwa ni ishara ya udhamini wa Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa unaotegemewa kuanza leo jijini Mwanza na unaotarajiwa kufunguliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania – John Magufuli. Wa pili kushoto ni Mkuu wa KItengo cha Huduma za Serikali – NMB – Vicky Bishubo na Katibu Mkuu wa ALAT – Elirehema Kaaya. NMB ndiye Mdhamini Mkuu wa Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa.
Mwenyekiti wa ALAT Taifa - Mh Gulamhafeez Mukadam akiondoka kwa mbwembwe na cheki ya mfano ya shilingi Milioni 150 aliyopewa na Afisa Mkuu wa Wateja Wadogo na wa Kati – filbert Mponzi kama ishara ya udhamini wa Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa unaotegemewa kuanza leo jijini Mwanza na unaotarajiwa kufunguliwa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania – John Magufuli. Wanaoangalia ni Katibu Mkuu wa ALAT - Elirehema Kaaya wa pili na Mjumbe wa Kamati Tendaji ya ALAT Mh Zaynab Vulu. NMB ndiye Mdhamini Mkuu wa Mkutano Mkuu wa ALAT Taifa. 


Benki ya NMB imesaidia Zaidi ya shilingi Milioni 150 kwaajili ya Mikutano Mikuu ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa (ALAT) kwa miaka mitano mfululizo huku wakiahidi kuendelea kushirikiana na serikali za mitaa nchini kutatua changamotoimbalimbali.

Afisa Mkuu wa Wateja Wadogo na wa Kati – Filbert Mponzi aliyasema hayo juzijijini Mwanza wakati akikabidhi udhamini wa Benki hiyo kama mdhamini Mkuu wawa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa ALAT unaoanza leo katika Hoteli ya MalaikaBeach jijini Mwanza.

Mponzi alisema kuwa Benki hiyo inatambua mahusiano ya kibiashara yaliyopokati ya NMB na ALAT kupitia Zaidi ya halmashauri 180 ambapo Benki inashirianakukusanya mapato ya Serikali huku akisema kusema kuwa taasisi hiyo ni mmbiawa karibu na serikali, hivyo mahusiano ya NMB na ALAT yameanza mudamrefu uliopita.

“Tunaishukuru sekretariet ya Alat pamoja na wajumbe wote kwa kuendelea
kutoa ushirikiano, kufanya biashara pamoja na sisi kama benki tumekuwa
tukiendelea kuboresha huduma zetu ili kuweza kuhudumia serikali kuu
pamoja na serikali za mitaa,” alisema Mponzi.

“Tumepeleka huduma zetu nchi nzima huku tukizifikia Zaidi ya halmashauri 180tukiwahudumia katika Nyanja mbalimbali za kibenki kuanzia wafanyakazi,wafanyabiashara na wajasiliamari na pia madiwani nah ii inaonyesha utayariwetu wa kuhudumia Serikali za mitaa.” Alisema Mponzi.

Mwenyekiti wa ALAT taifa – Gulamhafeez Mukadam ameishukuru Benki ya NMBkwa kuonyesha kujali Serikali za mitaa na mchango wa mwaka huu unaonyeshadhamira na ushirikiano wa kweli kati ya taasisi mbili.

Mheshimiwa Mukadam aliongeza kuwa jamii za Serikali za mitaa na mamlaka zakebado zinakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinahitaji kushikwa mkono nataasisi kama NMB kwaajili ya kusaidiana kutatua changamoto hizo.

Aliiomba pia Benki ya NMB kuangalia namna ya kuangalia upya misaada yakeinayotolewa kwa jamii kupitia uwajibikaji kwa jamii (CSR) akiomba Benki kuanzakusaidia jambo ambalo mwisho linakuwa kubwa kuliko misaada midogo midogoambayo inaweza ikawa na mchango mdogo kwenye jamii.

Mukadam alitoa mfano wa misaada ya vifaa vya ujenzi mashuleni na
mahospitalini na kusema kuliko kusaidia vifaa vya kuezekea, ichukue mradi mzimakama ni ujenzi wa darasa mpaka unakamilika kwa manufaa ya jamii.

“Nafikiria Benki inaweza sasa ikabadiri muelekeo wake kuhusu misaada
mbalimbali kwa jamii, kwa kuhakikisha wanachukua mradi hata mmoja mkubwakwenye wilaya na kuhakikisha wanaukamilisha kwa usimamizi wao ambao utaletaile thamani halisi ya fedha wanazotoa.” Alisema.

Mjumbe wa Kamatiu Tendaji ya ALAT na Meya wa SUmbawanga – Justine
Malisawa aliishukuru Benki ya NMB kwa kuleta mfumo wa ukusanyaji mapato yahalmashauri kielektroniki na kuisifia kuwa imeleta mafanikio makubwa kwamapato ya Serikali kuongezeka tofauti na ilivyokuwa zamani hasa ndani ya miakahii mitatu.

Maneno ya Bwana Malisawa yaliungwa mkono na Mbunge wa Viti Maalumu waKisarawe na Mjumbe wa Kamati tendaji ya ALAT – Mh Zaynab Vuli huku akisemaBenki hiyo imejipambanua kwa kufika maeneo ambayo Benki zingine hazijafika.

Mh Vulu aliiomba Benki hiyo kupunguza riba na kutoa mikopo nafuu kwa wafanyabiashara wadogo hasa wale wanaofanya biashara zao vijijini ili kusaidiamaendeleo ya mtu mmoja mmoja nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...