Na Said Mwishehe,Michuzi Blog

NAIBU Waziri wa Kilimo amesema anafahamu changamoto zilizpo kwenye sekta ya kilimo, hivyo atashirikiana na Waziri wa Kilimo kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi wa changamoto zilizopo kwenye sekta hiyo.

Bashe ameyasema hayo leo Ikulu jijini Dar es Salaam baada ya kula kiapo mbele ya Rais Magufuli ambapo amesema kuwa anaifahamu sana sekta ya kilimo kutokana na Spika kumteua kuwa mjumbe katika kamati.

"Wanyonge katika nchi hii wako katika eneo la kilimo na anafahamu changamoto zilizopo kwenye sekta ya kilimo na sasa nitakwenda kushirikiana na viongozi wengine kutatua changamoto.

"Nitatumia kila aina ya uwezo wangu kwa kushirikiana na Waziri wa Kilimo kutafuta ufumbuzi wa changamoto za kilimo,"amesema Bashe na kuongeza sekta ya kilimo imebeba sehemu kubwa ya wananchi ambao wanategemea kilimo, hivyo lazima sekta hiyo isimamiwe vizuri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...