Rais
wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kesho Jumamosi tarehe 13
Julai, 2019 atafanya Ziara Binafsi ya siku 1 moja hapa nchini.
Mhe.
Rais Museveni atamtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt.
John Pombe Magufuli kijijini kwake Mlimani katika Wilaya ya Chato Mkoani Geita.
Akiwa
Chato, Mhe. Rais Museveni atafanya mazungumzo na mwenyeji wake Mhe. Rais
Magufuli.
Gerson
Msigwa
Mkurugenzi
wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato
12
Julai, 2019
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...