Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiwakaribisha Viongozi wa Dini kwa ajili ya Kongamano la kujadili namna Viongozi hao wanavyoweza kusaidia katika mapambano dhidi ya Ugojwa wa Kifua Kikuu (TB)  katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam. Kongamano hilo pia lilihudhuriwa na Wajumbe wa Mtandao wa Wabunge wa Kupambana na  Ugojwa wa Kifua Kikuu wakiongozwa na Mwenyekiti wa Mtadao huo Mhe. Oscar Mkasa.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na Viongozi wa Dini wakati wa Kongamano la kujadili namna Viongozi hao wanavyoweza kusaidia katika mapambano dhidi ya Ugojwa wa Kifua Kikuu (TB)  katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Mtandao wa Wabunge wa Kupambana na  Ugojwa wa Kifua Kikuu,  Mhe. Oscar Mkasa akizungumza wakati wa Kongamano hilo lililowahusiha Viongozi wa Kidini ili  kujadili namna wanavyoweza kusaidia katika mapambano dhidi ya Ugojwa wa Kifua Kikuu (TB).
 Kaimu Meneja Mpango wa Taifa wa kudhibiti Ugojwa wa Kifua Kikuu na Ukoma, Bw. Dues Kamara akiwasilisha mada  wakati wa Kongamano la kujadili namna Viongozi wa Kidini wanavyoweza kusaidia katika mapambano dhidi ya Ugojwa wa Kifua Kikuu (TB)  katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.
 Mwekahazina wa Mtandao wa Wabunge wa Kupambana na  Ugojwa wa Kifua Kikuu,  Mhe. Kimirembe Lwota  akizungumza wakati wa Kongamano hilo lililowahusiha Viongozi wa Kidini ili  kujadili namna wanavyoweza kusaidia katika mapambano dhidi ya Ugojwa wa Kifua Kikuu (TB).
Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai, (katikati ya waliokaa) katika picha ya pamoja na Viongozi wa Dini, Wabunge  wa Mtandao kupambana na TB na wadau katika mapambano dhidi ya TB    wakati wa Kongamano la kujadili namna Viongozi wa Dini wanavyoweza kuwasaidia katika mapambano dhidi ya Ugojwa wa Kifua Kikuu (TB)  lilofanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha kutoka kulia waliokaa ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wabunge wa Kupambana na  Ugojwa wa Kifua Kikuu,  Mhe. Oscar Mkasa, Askofu Mkuu Mwandamizi wa Jimbo Katoliki la Dar es Salaam, Yuda Thaddeus Ruwa’ichi, Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zuberi, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam, Alhadi Mussa Salum na Makamu wa Rais wa Baraza la Maskofu Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Flavian Kassala.PICHA NA BUNGE

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...