Taasisi ya Young Scientists Tanzania(YST) inatarajia kufanya maonyesho ya Wanasayansi chipukizi kuanzia Julai 31 mpaka adosti 1 katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Waandishi wa habari mapema leo jijini Dar es Salaam Mwneyekiti w abodi ya YST nchini Profesa Yunus Mgaya amesema kuwa wanafunzi wanaopata fursa ya kushiriki maonyesho aya walipata fursa ya kuboresha ujuzi wao wa kisayansi kupitia mango wa uwezeshaji ulioendeshwa na wanasayansi washauri .

"kwa siku mbili wanasayansi chipukizi wataonyesha kazi zao katika nyanja mbalimbali za sayansi kama kemia, fizikia na hesabu ,biology mazingira na sayansi ya jamii na tekonolojia ,kazi hizi za kisayansi hasa ziwe zimejikitakatika utatuzi wa matatizo katika afya ,Kilimo, usalama wa chakula ,mawasiliano na usafirishaji " Amesema Prof Mgaya.

amesema wanasayansi watakaokuwa na ugunduzi mzuri watazawadiwa pesa taslim na medali wanasayansi wanne watapewa udhamini wa kusoma chuo kikuu na shirika la Karim mjee Jivanjee Foundaton.

Washindi wa jumla wataiwakilisha Tanzania kwenye Maonesho ya kimataifa ya Eskom Expo Young Scientists jijini Johannesburg Afrika Kusuni Oktoba mwaka huu.
Mwenyekiti wa bodi wa Tasisi ya Young Scientists Tanzania(YST), Prof Yunus Mgaya akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya kilele cha Maonesho ya tisa ya wanasayansi chipukizi yatakayofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere Convention Centre kuanzia Julai 31 mpaka Agosti 1 mwaka 2019.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)

Mwanzilishi Mwenza wa YST Nchini Dr.Gosbert Kamugisha (katikati) akieleza namna wanafunzi walioshiriki katika maonyesho hayo katika kipindi cha nyuma fursa walizopata ikiwemo ufadhili wa masomo ya kusoma elimu ya juu nje ya nchi.kushoto Mwenyekiti wa bodi wa Tasisi ya Young Scientists Tanzania(YST), Prof Yunus Mgaya kulia ni Mwanzilishi wa YST,Joseph Clowry.
 waandishi wa habari  wakimsiliza Mwenyekiti wa bodi wa Tasisi ya Young Scientists Tanzania(YST), Prof Yunus Mgaya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...