Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv

KIWANDA Cha Wazalendo cha Tropical Industies wamemshukuru Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa kuwapa fursa wamiliki wa viwanda ambao ni wazalendo kuuza bidhaa zao kwa urahisi mkubwa.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Kiwanda hicho, Charles Mlawa katika maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Michuzi TV, Mlawa amesema kiwanda chao kinajishugulisha na utengenezaji wa transfoma, nyaya za umeme za usambazaji na nyaya za usafirishaji zikizalishwa hapa nchini.

Mlawa amesema, amemshukuru Rais kwa fursa aliyoitoa kwa wazalendo kuweza kufanya biashara kwani kipindi cha nyuma walijaribu kufanya jitihada za kuuza kwa wateja wa ndani ilishindikana.

“Kauli ya Rais ya Tanzania ya Viwanda kuelekea uchumi wa kati imesaidia sana,wao kama kiwanda wamenufaika kwa kupata wateja wa ndani na nje ya nchi,”amesema Mlawa.

Aidha, amesema ndani ya miaka mine ya Dkt John Pombe Magufuli kwa vitendo na kwa kuzalisha bidhaa zenye ubora tena kikiwa ni kiwanda cha wazalendo kwa asilimia 100.

Ametoa rai kwa waanzania kuunga mkono bidhaa zinazotengenezwa na watanzania wenzao kwani zina ubora mzuri kama ule wa nje.
Mhandisi wa Kiwanda cha Tropical Industries Jacob Shirima akielezea namna wanavyoanza kutengeneza transfoma kuanzia hatua ya kwanza hadi linapokamilika katika banda lao liliopo ndani ya maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba kwenye Viwanja vya Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Meneja Mauzo wa Kiwanda cha Tropical Industries Rigobert Manega akielezea aina za nyanya wanazozitengeneza kutoka kwenye Kiwanda chao kinachopatikana Jijini Dar es salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...