Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la mkuranga mkoani Pwani mh ABDALLAH H ULEGA alifanya kikao na watendaji wa vijiji na kata zote zilizo katika Jimbo lake la mkuranga,

Ajenda kuu ya kikao hicho ilikuwa ni tathmini ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi wa chama Cha mapinduzi na maendeleo Kwa wananchi wilayani hapo,

Pi kikao hicho kilijikita katika kujadili Kero na changamoto mbalimbali Ktk utekelezaji wa kazi zao ili kurahisisha maendeleo kwa wananchi Mkuranga.

Watendaji hao pamoja na kueleza Baadhi ya Changamoto chache katika utendaji wao kazi wametoa pongezi Kwa Mbunge huyo wa mkuranga Kwa jinsi wanavyoshirikiana nae vizuri na kupongeza uchapakazi wake uliotukuka Kwa kuwapigania wanamkuranga ktk kuwaletea maendeleo wananchi wake na kuahidi kutoa ushirikiano kwake pale itakapohitajika Kwa maslahi mapana ya wananchi,

Vile vile watendaji hao hawakusita kuipongeza serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais JOHN POMBE MAGUFULI na watumishi wake wote Nchini Kwa uwajibikaji na uchapaji kazi na Nidhamu katika kazi.

Mh Abdallah Hamis Ulega ambaye ni Mbunge wa Jimbo la mkuranga pia hakusita kuwapongeza watendaji hao Kwa jinsi wanavyowajibika na kuwataka wafanye kazi zao naye Yuko pamoja nae kwaajili ya kuwatumikia wanamkuranga wote bila kujali itikadi zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...