Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linapenda kuutaarifu Umma wa  Tanzania  kwamba, Wamiliki wa majengo na Wafanyabiashara waliofanyiwa ukaguzi wa kinga na tahadhari dhidi ya majanga ya moto na kukidhi vigezo vya usalama wa moto, kufika au kuwasiliana na Ofisi ya Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa husika au kituo cha Jeshi hilo kilicho karibu yake, kwa ajili ya kuchukua Hati ya Usalama dhidi ya Moto (Fire Safety Certificate).
Cheti cha Usalama dhidi ya Moto kinapatikana baada ya kufanyiwa ukaguzi wa kinga na tahadhari dhidi ya majanga kwenye majengo. Ukaguzi huo unafanyika kwa mujibu wa Sheria namba 14 ya mwaka 2007, ikisomwa pamoja na Kanuni ya Vyeti na Usalama wa moto ya Mwaka 2008 na marekebisho ya mwaka 2014 (Fire and Rescue Force Safety Inspections and Certificates Regulations of 2008 GN.106 and its Amendment GN 63 of 2014.) Pamoja na Kanuni ya tahadhari dhidi ya moto kwenye majengo ya mwaka 2015 (Fire and Rescue Force Fire Safety Precaution in Building Regulations of 2015 GN 516.)
Jeshi la Zimamoto na Uokoaji linatoa rai kwa Umma kujenga tabia ya kutembelea vituo vilivyo karibu kwa ajili ya kupata ushauri pamoja na kuchukua hati za usalama dhidi ya moto.
Imetolewa na,

Kitengo cha Habari, Uhusiano na Elimu kwa Umma Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,
Makao Makuu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...