Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akizungumza na waombolezaji wakati alipowaongoza katika Ibada na kuaga mwili wa mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Richard Kalinga, nyumbani kwa marehemu jijini Dodoma, Julai 22, 2019. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maadhimisho, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mohammed Kiganja.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama akitoa pole kwa familia ya mtumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Marehemu Richard Kalinga, baada ya kuwaongoza waombolezaji katika Ibada ya kumwombea marehemu na kutoa heshima za mwisho, nyumbani kwa marehemu jijini Dodoma Julai 22, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...