Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

Shirikisho la Mpira Afrika CAF wametoa ratiba ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika (CCL) ambapo wawakilishi wa Tanzania kwenye michuano hiyo Simba na Yanga zikipangiwa timu kutoka ukanda wa Jangwa la Sahara.

Mabingwa wa Tanzania Simba wataanzia ugenini dhidi ya timu ya UD do Songo ya Msumbiji kati ya tarehe 09/10/11 Agosti 2019 nchini Msumbiji.

Mshindi wa mchezo kati ya Simba na UD do Songo atacheza na mshindi kati ya Nyasa Big Bullets ya Malawi na Platnumz ya Zimbabwe.

Wawakilishi wengine wa michuano hiyo Yanga wataanzia nyumbani dhidi ua Township Rollers mchezo utakaochezwa kati ya tarehe 09/10/11 Agosti 2019 na baadae kurudiana nao nchini Botswana.

Mshindi wa mchezo huo atamsubiri mshindi kati ya Green Mamba Eswatin na Zesco ya Zambia.Kwa upande wa wawakilishi kutoka Zanzibar, KMKM watarusha karata yao ya kwanza kwa Desportivo De 1 Agosto ya Angola na mshindi wa mchezo huo atamsubiri na Green Eagles ya Zambia dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.

Kwa kuanzia msimu wa mwaka 2019, CAF wameongeza timu kutoka Tanzania kwa upande wa Klabu Bingwa ni timu mbili na Shirikisho timu mbili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...