Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela amefungua rasmi nyumba mpya ya kuabudia (kanisa la jipya AICT Kahama Mjini) lililogharimu jumla ya shilingi milioni 900 (902,397,070/=).

Ufunguzi wa kanisa hilo bora na la kisasa lililopo Nyihogo Mjini Kahama umefanyika leo Jumapili Agosti 25,2019 na kuhudhuriwa na maelfu ya viongozi,waumini na wageni mbalimbali kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga.

Akizungumza wakati wa kuweka wakfu na kufungua jengo hilo jipya,Askofu Magwesela alisema ni jengo bora na la kisasa huku akiwasisitiza waumini na kutumia jengo hilo kumwabudu Mungu.

"Kwa heshima ya Mungu nalifungua na kuliweka wakfu jengo hili. Nyumba hii ni kwa ajili ya ibada pekee,naomba mlitumie kwa maksudi yaliyokusudiwa",amesema. 

Akisoma taarifa ya ujenzi,Katibu wa Kanisa la AICT Kahama Mjini,Charles Pambe amesema kanisa la AICT Kahama Mjini limeanzishwa tarehe 15 Novemba,1975 na mpaka sasa limefungua Pastoreti tisa mjini Kahama na Pastoreti mama ya Kahama,Mlima Sayuni,Mhongolo,Mhungula,Nyakato,Lugela,Majengo,Mbulu na Mwendakulima.

Amesema wamejenga jengo jipya kisasa la kuabudia lililotokana na michango ya waumini ambapo lina mahitaji muhimu ikiwa ni pamoja na ofisi sita,vyoo,sehemu ya kubatizia na maombi ya faragha,mabenchi,meza hivyo mpaka jengo linafunguliwa limegharimu jumla ya shilingi 902,397,070/=.

Amebainisha kuwa mbali na kujenga kanisa jipya pia wamejenga nyumba ya kisasa ya Mwinjilisti,madarasa mawili na ofisi zake,bwalo la kulia chakula na kanisa linaendelea na utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa shule ya msingi 'English Medium School',ujenzi wa shule ya sekondari na zahanati na ukamilishaji wa hosteli ya kanisa. 
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akiendesha ibada ya kufungua na kuweka wakfu jengo jipya la kuabudia katika kanisa la AICT Kahama Mjini leo Jumapili Agosti 25,2019. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akiendesha ibada ya kufungua na kuweka wakfu jengo jipya la kuabudia katika kanisa la AICT Kahama Mjini.
Maaskofu wa kanisa la AICT wakiendelea na ibada ya ufunguzi na uwekaji wakfu jengo jipya la kanisa la AICT Kahama Mjini. Aliyeshikilia kipaza sauti ni Askofu wa Dayosisi ya Shinyanga, Zakayo Bugota.
Muonekano wa jengo jipya la kanisa la AICT Kahama Mjini.
Muonekano wa jengo jipya la kanisa la AICT Kahama Mjini.
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo jipya la kuabudia katika kanisa la AICT Kahama Mjini.
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akikata utepe wakati wa kufungua jengo jipya la kuabudia katika kanisa la AICT Kahama Mjini.
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akifungua jengo jipya la kuabudia katika kanisa la AICT Kahama Mjini.
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akifungua mlango kuingia ndani ya jengo jipya la kuabudia/kanisa la AICT Kahama Mjini.
Katibu wa Kanisa la AICT Kahama Mjini,Charles Pambe akisoma taarifa ya ujenzi wa kanisa jipya la AICT Kahama Mjini ambalo limegharimu jumla ya shilingi milioni 900.
Katibu wa Kanisa la AICT Kahama Mjini,Charles Pambe akisoma taarifa ya ujenzi wa kanisa jipya la AICT Kahama Mjini ambalo limegharimu jumla ya shilingi milioni 900.
Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akizungumza wakati wa kufungua kanisa jipya la AICT Kahama Mjini na kuwasisitiza waumini kutumia kanisa hilo kumwabudu Mungu pekee.


Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akizungumza wakati wa kufungua kanisa jipya la AICT Kahama Mjini.




Askofu wa Dayosisi ya Shinyanga, Zakayo Bugota akizungumza wakati wa ufunguzi wa kanisa jipya la AICT Kahama Mjini.




Askofu wa Kanisa la AICT Dayosisi ya Tabora, Silasi Kezakubi akiweka wakfu benchi katika kanisa jipya la AICT Kahama Mjini.




Askofu Mkuu wa Kanisa la AICT nchini,Musa Masanja Magwesela akizungumza baada ya kufungua kanisa jipya la AICT Kahama Mjini.




Viongozi mbalimbali wa Kanisa la AICT wakiwa kanisani wakati wa kufungua kanisa jipya la AICT Kahama Mjini. Maaskofu wakiwa wamekaa jukwaa kuu wakati wa ibada ya Jumapili baada ya kufungua kanisa jipya la AICT Kahama Mjini.


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...