Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akimkabidhi kitabu cha Mpango Mkakati wa kutokomeza Ukatili wa Kijinsia dhidi ya wanawake na watoto Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri wakati wa uzinduzi wa Kamati ya ulinzi ya wa wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akizindua Kamati ya ulinzi ya wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akiwasalimia wakazi wa Wilaya ya Kigambo wakati wa uzinduzi wa Kamati ya ulinzi ya wa wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na uzinduzi wa Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatiliwa Kijinsia Tanzania sasa basi. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akizungumza na wakazi wa Wilaya ya Kigambo ni wakati wa akizindua Kamati ya ulinzi ya wa wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na uzinduzi wa Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akiangalia bidhaa zinazotengenzwa na wanawake wa wilaya ya Kigamboni wakati wa uzinduzi wa Kamati ya ulinzi ya wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na uzinduzi wa Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi. 
Baadhi ya wakazi wa Wilaya ya Kigamboni wakifuatili hotuba za viongozi, mada na burudani wakati wa uzinduzi wa Kamati ya ulinzi wa wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi. 
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt Faustine Ndugulile akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri pamoja na wadau wengine mara baada ya kuzindua Kamati ya ulinzi wa wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja Ukatili wa Kijinsia Tanzania sasa basi. Picha na Kitengo cha Mawasiliano WAMJW 



Na Mwandishi Wetu WAMJW 

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amewaagiza watendaji wa Wilaya ya Kigamboni kuhakikisha Kamati za ulinzi wa Wanawake na watoto zinatekeleza majukumu yake ipasavyo kwa kuisadia jamii ya wanakigamboni kupambana na vitendo vya ukatili wa kijinsia . 

Dkt. Ndugulile amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa akizindua Kamati ya ulinzi ya wanawake na Watoto ya Wilaya ya Kigamboni pamoja na Kampeni mpya ya Kitaifa ya kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto ijulikanayo kama Twende Pamoja inayolenga kushirikisha wanaume na wanawake kwa lengo la kutoa elimu kwa jamii kupitia mbinu anwai. 

Aidha Dkt. Ndugulile amesisitiza kuwa Kamati hizo ikisimamiwa vizuri itakuwa nuzo bora katika mapambano dhidi ya vitendo vya kikatili vinavyozidi kushamiri kila siku nchini katika jamii na familia zetu. 

Ameongeza kuwa kuwepo kwa elimu bure nchini kwa kiasi kikubwa kumepunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake ikiwemo mimba na ndoa za utotoni pamoja na uwepo wa Sheria inayotoa adhabu ya kifungo cha miaka 30 jela kwa anayebainika kufanya vitendo hivyo. 

”Ni matarajio yangu kwamba kampeni hii ya Kupinga Ukatilili wa Kijinsia Kitaifa italeta mabadiliko makubwa kupitia jumbe mbalimbali zilizoandaliwa kupitia muziki, machapisho, nyimbo, shuhuda na Semina zitakazokuwa zinaendelea kutolewa kwenye majukwaa mbalimbali kipindi cha kampeni’’ alisema Dkt. Ndugulile. 

Dkt. Ndugulile pia ameagiza kutafutwa kwa wale waonafanya vitendo vya kikatili katika wilaya ya Kigamboni na Tanzania kwa ujumla na vyombo husika kusimamia na kuhakikisha wanawake na watoto wanapata haki zao. 

Akizungumzia hali ya ukatili wa kijinsia nchini Dkt. Ndugulile amesema taarifa ya hali ya Uhalifu nchini ya Mwaka 2017 inaonesha kuwa jumla ya watu 41,416 waliofanyiwa ukatili wa kijinsia walitoa taarifa kwenye vituo vya polisi ikilinganishwa na watu 31,996 waliofanya hivyo mwaka 2016. 

Dkt. Ndugulile ameyataja baadhi ya matukio ya ukatili yaliyotolewa taarifa kuwa ni ubakaji, vipigo, matusi, ulawiti, kutupa watoto, ukeketaji na kuwapa mimba wanafunzi na kuongeza kuwa kati ya mataukio hayo 41,416 yaliyotolewa taarifa mwaka 2017 matukio 27,703 sawa na asilimia 67 yalifanywa dhidi ya wanawake na watoto. 

Dkt. Ndugulile ameongeza kuwa asilimia 40 ya wanawake wa umri kati ya miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili au kingono mara moja au zaidi katika kipindi hicho cha maisha wakati wanawake asilimia 20 wenye umri miaka 15-49 wamefanyiwa ukatili wa kimwili katika kipindi cha miezi 12 iliyopita. 

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Mhe. Sarah Msafiri amesema kuwa Serikali ya Wilaya itahakikisha wanapambana na vitendo vya kikatili na amewaomba wanawake kutoa taarifa ya vitendo hivyo na kuwataka kutofumbia macho vitendo hivyo na kuacha vipite kwa mwavuli wa ndoa. 

“Sisi Serikali tunaheshimu ndoa na dini zote ila tunaangalia uhai wa mwananchi hivyo wanawake wenzangu nawaomba ndoa zisiwe sababu ya kuendelea kufanyiwa vitendo vya kikatili na kuachana inawezekana” alisema Mhe. Sarah 

Naye mmoja wa wnawake aliyefanyiwa vitendo vya kikatili Bi. Lucy Sanga ameishukuru Serikali ya Wilaya ya Kigamboni kwa kumsaidia kupambana na vitendo vya manyanyaso ambavyo anafanyiwa na mume wake. 

“Mume wangu amekuwa akininyanyasa sasa kwa muda mrefu na imefikia hatua ya kuficha vyombo vya kupikia na kunihamisha chumba chetu cha kukaka na kumleta mama yake mzazi kutoka Musoma na yeye analala humo na me nalala kwenye chumba cha watoto” alilalama Bi. Lucy

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...