Moja ya mwanzilishi wa mpango wa "Her Africa", Bi. Zena Tenga (kushoto) na mwezeshaji Bi Erica Zilinde (kulia) wakiongea na wanafunzi wa kike wa kidato cha 1 na 2 kutoka Chang'ombe secondary kuhusu fikra potovu na miiko juu ya hedhi kama sehemu ya kampeni ya mpango huo iitwayo "Hedhi yangu, Furaha yangu" inayolenga kuelimisha wasichana juu ya hedhi salama na pia kutoa vifaa vya hedhi kwa wasichana nchini Tanzania. 
Wanafuzi wa kike wa kidato cha kwanza na cha pili kutoka shule ya secondary ya Chang'ombe wakifurahia mifuko yenye vifaa vya hedhi waliyo pewa na mpango wa "Her Africa" kama sehemu ya kampeni yao iitwayo "Hedhi yangu, Furaha yangu" inayolenga kuelimisha wasichana juu ya hedhi salama na pia kutoa vifaa vya hedhi kwa wasichana nchini Tanzania. Jumla ya mifuko 85 ilitolewa kwa wasichana hao.
Daktari Elaina Lengereli na nesi Ziada Kabanda kutoka Sisa Community Center wakiongea na wanafunzi wa kike wa kidato cha 1 na 2 kutoka Chang'ombe secondary kuhusu hedhi salama na afya ya msichana kama sehemu ya kampeni ya mpango wa "Her Africa" iitwayo "Hedhi yangu, Furaha yangu" inayolenga kuelimisha wasichana juu ya hedhi salama na pia kutoa vifaa vya hedhi kwa wasichana nchini Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...