Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii

MKUU wa Majeshi nchini, Jenerali Venance Mabeyo amewataka Wanajeshi ambao wanaendelea kutumikia taifa kufuata misingi na maadili ya Jeshi ili wanapomaliza muda wao wa kazi waagwe kwa heshima. 

Mabeyo amesema hayo wakati wa hafla ya kuwaaga Majenerali 9 ambao wamestaafu utumishi wa Jeshini ambapo amesema mwanajeshi ili apewe heshima anatakiwa awe na nidhamu awapo kazini. 

Amesema Majenerali hao ambao wamestaafu kwa muda wa miaka mitatu wataendelea kuwa washauri katika jeshi la akiba. "Ambao bado wapo makazini wajitaidi kuwa na nidhamu ili wakati wanastaafu wapewe heshima kama hii ya leo,”amesema .

“mwanajeshi akistaafu uagwa kiheshima pindi anapostaafu tofauti na ukifukuzwa uwezi kupewa heshima”
Nao Baadhi ya Majenerali ambao wamestaafu waliwataka wanajeshi ambao wamebaki kuitumikia nchi kwa moyo mmoja. 

Joyce Kabatiambaye ni mmoja wa Majenerali hao aliwahasa wazazi na walezi kuacha dhana potofu kuwa watoto wa jinsia ya kike awawezi kuwa wanajeshi. Dk.Denis Janga ameelza katika kipindi chake cha utumishi wa jeshi alikua Daktari na alishiriki Vita vya Uganda hivyo aliwahasa wananchi kulinda amani iliyopo na kuepukana na migogoro kwa vita si nzuri
"Niliyoyashuhudia wakati wa ile vita sitaki kuona yanatokea maana watu walipata shida sana "amesema

Aidha wanajeshi hao wastaafu wamemshukuru mwenyezi mungu kwa kuwasaidia kumaliza kipindi chao salama na kupata heshima ya kuagwa kwa Amani.Wanajeshi walioagwa ni P6693 Meja Jenerali Issa Suleiman Nassor mstaafu, P3726 Meja Jenerali Gaudence Salim Milanzi mstaafu, P3649 Meja Jenerali Denis Raphael Janga mstaafu, P7696 Brigedia Jenerali Zoma Mathic Kongo mstaafu, 

P7833 Brigedia Jenerali Nicodems Elias Mwangela mstaafu, P6090 Brigedia Jenerali Charo Hussein Yateri mstaafu, P8019 Brigedia Jenerali Raymond Kusirie Mwanga mstaafu, P8023 Brigedia Jenerali Juma Hidaya Mwinula mstaafu na PW 0131 Brigedia Jenerali Joyce Luli Kabati mstaafu.
 Mameja Jenerali, kutoka (kushoto) Gaudence Milanzi, Issa Suleiman na Denis Raphael, wakitoa heshima wakati wa gwaride maalumu la kuwaaga baada ya kustaafu katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Kambi ya Twalipo, Dar es Salaam.
 Mkuu wa Majeshi Nchini Jenerali Venance Mabeyo akiwa kwenye picha ya pamoja na Wanajeshi waliostaafu na kuagwa kwa heshima leo kwenye hafla fupi iliyofanyika kwenye kambi ya Twalipo, Jijini Dar es Salaam
 MKUU wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo, akimkabidhi kitambulisho cha kustaafu kazi, Meja Jenerali, Issa Suleiman Nassor wakati wa hafla ya kuwaaga Mameja Jenerali na Mabrigedia Jenerali , iliyofnayika katika Kambi ya Twalipo Dar es Salaam.
 MKUU wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo, akimkabidhi kitambulisho cha kustaafu kazi, Meja Jenerali, Gaudence Milanzi wakati wa hafla ya kuwaaga Mameja Jenerali na Mabrigedia Jenerali , iliyofanyika katika Kambi ya Twalipo Dar es Salaam.
 MKUU wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo, akimkabidhi kitambulisho cha kustaafu kazi, Meja Jenerali, Joyce Kabati wakati wa hafla ya kuwaaga Mameja Jenerali na Mabrigedia Jenerali , iliyofanyika katika Kambi ya Twalipo Dar es Salaam.
 Gwaride la heshima kwa wastaafu wakati wa hafla ya kuwaaga Mameja Jenerali na Mabrigedia Jenerali , iliyofanyika katika Kambi ya Twalipo Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...