Na Said Mwishehe,Michuzi TV 

NAIBU Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashanta Nditiye amesema Serikali inao mkakati wa kupeleka bungeni muswada kwa ajili ya kulinda taarifa binafsi za mtu, lengo likiwa ni kulinda mawasiliano binafsi na kufanya udukuzi.

Mhandisi Nditiye ameyasema hayo leo Agosti 14 , mwaka 2019 wakati anazungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam alipokuwa akielezea mikakati ya wizara hiyo kwa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika(SADC).

Hivyo pamoja na kutoa maelezo ya mikakati hiyo ya Wizara, Mhandisi Nditiye aliulizwa iwapo Wizara imeweka mkakati wowote kudhibiti udukuzi wa kuingilia taarifa za mtu binafsi na namna ilivyojipanga kukabiliana na uhalifu wa mtandaoni.

“Matumizi sahihi ya mawasiliano nchini bado yana changamoto na pamoja na juhudi zilizoweka kupambana na wote wanaochafua wenzao kupitia mawasiliano.Tutapeleka muswada wa sheria bungeni mwaka huu.

“Tunapambana na wote wanaochafua wenzao kwa mawasiliano ya simu, Mamlaka yetu ya Mawasiliano (TCRA) kwa kushirikiana na kitengo cha uhalifu wa mtandaoni (Cyber Crime) katika Wizara ya Mambo ya Ndani, tunashirikiana katika hili,” amesisitiza Mhandisi Ndetiye.

Hata hivyo kwa mujibu wa Mhandisi Ndetiye, amesema asilimia 98 ya mawasiliano ya ujanja ujanja wa kuunganisha simu za kimataifa zimedhibitiwa nchini.

Ameongeza sekta ya mawasiliano ni mtambuka na imeendelea kuchangia mapato ya Serikali kutoka asilimia 13.1 mwaka 2017 hadi asilimia 14.7 mwaka 2018 huku akieleza kipaumbele ni kuona inachangia zaidi.

Wakati huo huo Mhandisi Nditiye amesema kwa sasa nchini Tanzania watumiaji wa simu wamefikia milioni 43.6 na wa mtandao wa intaneti wamefikia watumiaji milioni 23.140.Hivyo sekta ya mawasiliano ikitumika vizuri ni muhimili mkubwa wa maendeleo ya uchumi nchini.

Kwa upande wa malengo ya kikanda, amesema nchi ya Tanzania inamkakati wa kuziunganisha nchi zote za jumuiya hiyo kwenye Mkongo wa Taifa kwa lengo la kuhakikisha nchi hizo zinakuwa na uhakika wa mawasiliano kwa ajili ya kuleta maendeleo.

Amefafanua tayari serikali ya Tanzania imeziunganisha nchi mbili za Zambia na Msumbiji na nne za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Uganda , Kenya, Burundi na Rwanda. “Mkakati uliopo kupitia Mkongo wa Taifa tunampango wa kuzifikia nchi zote za SADC”.

NAIBU Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashanta Nditiye akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam alipokuwa akielezea mikakati ya wizara hiyo kwa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika(SADC),ambapo pia kulifanyika hafla fupi ya uzinduzi wa machapisho matano yaliyotayarishwa na Kituo cha Utafiti kwa nchi za SADC.Picha na Michuzi JR.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...