Picha ya Amaury na Andrew Razafitrimo kutoka Madagaska
wakimkumbuka mama yao ambaye alifariki dunia katika shambulio la ugaidi 14 July 2016.

Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
TANZANIA ikiwa ni nchi mojawapo inayopingana na ugaidi na kuiweka Tanzania kuwa mahali salama pa kuishi leo duniani kote inafanyika kumbukumbu ya waathirika wa ugaidi ambao umewahi tokea duniani kote.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres  katika kumbukumbu ya kuwakumbuka waathirika wa ugaidi duniani kote amesema kuwa "Ninaomba sote tuangalie maisha ambayo yamebadilishwa milele kwa sababu ya ugaidi. Tujitolee kuwaonyesha waathirika wa matukio ya kugaidi kuwa  wao sio peke yao na  jamii ya umoja wa mataifa imesimama katika kumbukumbu hiyo  pamoja nao popote walipo duniani.

Ikiwa mataifa mengi yameathiriwa na ugaidi hata nchini za Afrika Mashariki zinawahanga wa matukio ya ugaidi hasa nchi ya Kenya leo ni kumbukumbu ya kuwakumbuka waathirika wa matukio hayo ambayo yanamaliza wanadamu kwa kiasi mkubwa.

Tuungane kwa pamoja katika kukemea ugaidi unaochukua maisha ya watu wengi na kusababisha yatima, na kuongeza balaa la umasikini  duniani kote.
Waathirika wa matukio ya kigaidi wasifikiri kuwa wapo peke yao dunia kwa ujumla imetenga siku ya leo ya Agosti, 21 kila mwaka kuwakumbuka watu walioathirika na matukio ya ugaidi nchini kote.

 Waathirika wanatakiwa kufarijiwa, kusamehana pamoja na kupewa msaada wa hali na mali, kijamii, kifedha pamoja na kisaikolojia ili kulinda utu wao.

Umoja wa mataifa unaungana na waathirika wote wa matukio hayo ili kuhakikisha  unahaki ya kutoa msaada katika nchi malimali ili kuzuia matukio ya kigaidi yanayoweza kujitokeza katika nchi mbalimbali ili kuchochea amani na upendo.

Katika kumbukumbu ya kuwakumbuka waathirika wa matukio ya ugaidi ni uzingatiaji katika uimarishaji wa wathirika na familia zao jinsi wameweza kukabiliana na kile ambacho kimefanya kubadili uzoefu wa maisha yao ili kusaidia uponyaji wa waathirika pamoja na kupambana kwa nguvu dhidi ya ugaidi.

Vyombo vya usalama hapa nchini vinaonekana kuwa mstari wa mbele katika kukabilia na ugaidi ili kuleta amani katika nchi yetu ikiwa Juni 19, 2019 katika ukurasa wa mitandao ya kijamii wa Umoja wa Mataifa ulipata fununu za kuwepo kwa shambulio la kigaidi nchini na Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) nchini Tanzania, Simon Sirro wakati akizungumza na gazeti la Mwananchi alisema kuwa  jeshi lake lilishapata fununu za shambulio hilo kabla Ubalozi wa Marekani kutoa tahadhari juu ya tukio hilo kupitia tovuti yake Juni 19,2019.

Kuhusu tahadhari iliyotolewa na ubalozi wa Marekani nchini Tanzania Sirro alisema: "hiyo ni taarifa kama taarifa nyingine, inaweza kuwa ya kweli au uongo, lakini sisi kama vyombo vya ulinzi huwa hatupuuzi jambo katika kukabiriana jambo lolote''.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...