Na Chalila Kibuda, Michuzi TV.

Waandaji wa Bonse Vibe Festival wamesema katika sikukuu ya Eid Alhaj wameanda burudani za asili kutoka kwa makundi mbalimbali ya wasanii ambao hawatawaungusha mashabiki wao.

Meneja wa Burdan wa Dar Live Rajab Mtenda amesema kuwa shoo ya kesho ni ya kukuta na shoka katika ukumbi wa Dar Live kutokana na walivyipanga wasanii watakaoshusha burdan hiyo.

Amesema kuwa tamasha hilo linaupekee linalotofautiana na matamasha mengine katika kuendeleza muziki wa asili nchini Tanzania.

Mkuu wa Uendeshaji wa LBM Victor Kaduma amesema kuwa tamasha hilo litabamba kwa siku kesho kwani hakuna tamasha lingine kwa siku hiyo.Nae Msanii Heri Samil (Mr Bluu)amesema kuwa katika sikukuu ya kesho mashabiki waje kuangalia show hiyo na kundi lake analosimamia.

Wasanii watakuwepa ni Mr Bluu, Hamisa Mobeto, Chid Benz, Easy Man pamoja na Mzee wa Bwaks.
Meneja wa Burdan wa Dar Live Rajab Mtenda akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na tamasha litakalofanyika Kesho katika Siku ya Eid Alhai katika ukumbi wa Dar Live jijini Dar es Salaam.
Msanii Heri Samil (Mr Bluu akizungumza na waandishi wa habari alivyojipanga katika tamasha litakalofanyika Kesho katika Sikukuu ya Eid Alhai katika ukumbi wa Dar Live jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Uendeshaji wa LBM Victor Kaduma akitoa maelezo namna walivyojipanga kufanikisha Tamasha hilo katika ukumbi wa Dar Live jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...