Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Hisham Hendi (kulia) akimkabishi Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia (Kusho ), mfano wa hundi yenye thamani ya shilingi za kitanzania bilioni 9, fedha ambazo zimetolewa na kampuni ya Vodacom Tanzania kudhamini ligi kuuTanzania bara kwa kipindi cha miaka mitatu (2019/2021), katika hafla fupi iliyofanyika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam jana.  Anayeshuhudia ni Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe.
Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, akizungumza na waandishi wa habari katika hafla ya kutangaza udhamini  wa ligi kuu ya Vodacom iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.  Kampuni ya Vodacom imetoa kiasi cha sh. bilioni 9 kudhamini ligi kuu ya Tanzania bara kwa kipindi cha miaka mitatu (2019/2021) kwa lengo la kuinua vijana wenye vipaji vya mpira wa miguu nchini na kuchochea maendeleo kwa ujumla. kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Hisham Hendi na Kulia ni  Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia.
 Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Hisham Hendi wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya udhamini uliotolewa na  kampuni Vodacom kwenda TFF kwa ajili ya Ligi kuu ya Tanzania Bara, katika hafla fupi iliyofanyika ofisi za makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam jana.  Kampuni ya Vodacom imetoa  kiasi cha sh bilioni 9 kudhamini ligi kuu Tanzania bara kwa kipindi cha miaka mitatu (2019/2021) kwa lengo la kuinua vijana wenye vipaji mpira nchini na kuchochea mendeleo kwa ujumla. Kulia ni  Rais wa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) Wallace Karia


Vodacom Tanzania kudhamini ligi kuu ya Tanzania kwa miaka mitatu
Agosti 23, 2019 – Dar es Salaam: Ligi kuu ya Tanzania yarudi kwa kishindo baada ya Vodacom Tanzania na shirikisho la soka TFF kufikia maridhiano na Vodacom kudhamini ligi hyo. Kampuni hiyo imesaini mkataba na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambao utawezesha shirikisho hilo la soka kupokea TZS bilioni 9 za udhamini kwa kipindi cha miaka mitatu (2019/2021), na kupelekea Vodacom kuendelea kuwa mdhamini mkuu wa ligi hiyo.

Ushirikiano na udhamini huo ulitangazwa katika hafla fupi iliyofanyika ofisi za makao makuu ya Vodacom, jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe, na umehusisha pande zote ambazo ni kampuni ya Vodacom Tanzania, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na bodi ya ligi.

Ligi kuu ya Tanzania ambayo sasa itaitwa Ligi kuu ya Vodacom itaanza tarehe 24 ya mwezi huu, ikitarajia kushuhudia jumla ya michezo 380 ikichezwa katika viwanja mbalimbali nchini na kushirikisha timu 20 zilizoko ligi kuu ya Tanzania bara.

Akizungumza katika hafla hiyo Dk Mwakyembe alisema serikali imepiga hatua kubwa katika kuwezesha vijana wenye vipaji mbali mbali nchini na alisisitiza umuhimi wa kuwekeza katika Vijana ili kuleta Maendeleo nchini. Pia aliipongeza Vodacom kwa kutia chachu juhudi za serikali katika kufanikisha malengo hayo.

 “Ukweli ni kwamba tupo katika wakati ambao tunahitaji kushirikiana na vijana katika kuleta maendeleo ya kijamii na kiuchumi, ambapo mpira wa miguu unaajiri mamia ya vijana hao. Uwekezaji uliofanywa na Vodaom siku hii ya leo ni moja ya ngao ya kuleta mabadiliko makubwa katika mpira wamiguu nchini, vile vile kuongeza ajira kwa vijana. Napenda kuwasihi wawekezaji kuwekeza katika michezo mbali mbali ili kufanya vijana wetu wawe wachangiaji wakubwa katika maendeleo ya uchumi,” aliongeza Mwakyembe.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Bwana Hisham Hendi amesema kuwa kampuni ya Vodacom iko mstari wa mbele katika kuunga mkono maendeleo na shughuli za mpira wa mguu hapa inchini hivyo leo ni siku ya furaha sana kwao. 

 “Tumedhamini ligi hii kwa zaidi ya miaka 9 na tumeona vipaji vingi vikiibuka na ligi kuongezeka umaarufu nchini na nje ya nchi ikufuatiliwa na mamilioni ya washabiki. Wote tumekubali kuwa wanamichezo ni mabalozi wazuri wa nchi yetu kama tulivyoona katika michuano ya AFCON iliyoisha hivi karibuni. Ni wajibu wetu kuhakikisha kuwa tunawaunga mkono katika kutambua na kukuza vipaji vyao kadri tutakavyo weza” alisema Hisham .

Bwana Hendi aliongeza kuwa amejivunia kampuni hiyo kurejea kuidhamini ligi kuu kwa kipindi kingine na kufafanua kuwa itaendelea kuwa mdau wa kukuza vipaji vya vijana kupitia michezo hapa Tanzania.

Pia aliweka wazi kwamba ligi kuu ya Vodacom inakuja na ofa kabambe kwa wateja wao pamoja na mashabiki wa mpira kupitia huduma ya SOKA LETU. “Pale mteja anapojiunga na SOKA LETU anapata dondoo mbali mbali za michezo, ikiwemo VPL na si hayo tu, sasa anapata nafasi ya kujishindia dakika au tiketi ya kwenda kutizama michuano itakayokuwa ikiendelea na zawadi nyingie kabambe,” alisisitiza Hendi.

Kwa upande wake Rais wa TFF, Wallace Karia, ameipongeza kampuni ya Vodacom Tanzania akisema kuwa anaamini, maendeleo ya sasa yatalenga zaidi katika kuunga mkono vipaji vipya na vilivyopo ndani ya nchi. “Kwa niaba ya TFF, napenda kuwashukuru Vodacom Tanzania kwa kuonyesha nia na kuendelea kuunga mkono mpira wa miguu nchini. Nasi tunaahidi kuendelea kuthamini vipaji vya wachezaji wetu na kuhakikisha tunapata mafanikio zaidi,” alisema Karia.


 “Ikiwa ni sehemu ya malengo yetu ya kuipeleka Tanzania katiza zama na malipo kwa njia ya kidigitali, Sasa wateja wetu wote na mashabiki wa mpira watanuua tiketi zao kupitia M-Pesa kutoka mtandao wowote hata mabenki. Kwa kweli ukiwa na Vodacom yajayo yanafurahisha,” alihitimisha Bw Hendi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...