Na, Editha Edward-Tabora 

Waumini wa dini ya kiislamu Mkoani Tabora leo wameungana na waumini wengine ulimwenguni kote kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha na kufanya Dua Kufuatia Vifo vya Watu zaidi ya 70 waliokufa kwa ajali ya Lori la mafuta kuwaka moto mkoani Morogoro na kuwaombea Majeruhi 46 wa ajali hiyo 

Katika Ibada hiyo muhimu iliyohudhuriwa na waumini wa kiislamu katika kwanja cha Alli Hassan Mwinyi, Sheikh mkuu wa Tabora Alhaj Ibrahimu Mavumbi akahudhurisha salamu za pole kwa ndugu na jamaa wa wafiwa na majeruhi wa ajali ya moto Mkoani Morogoro 

"Msiba huu ni wa kitaifa umepunguza nguvu Kazi kwa jamii wote hawa walikuwa na ndoto zao lakini Mauti imewakatiza wengine wemeacha watoto, Wajane niwape pole wale wote waliofikwa na msiba huo na tudumu katika Imani " Amesema Mavumbi

Pia Sheikh Mavumbi amewataka wananchi wote kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa nchini kote Kushiriki uchaguzi huo kwa Amani na utulivu Ili kuweza kupata viongozi kwa Amani 

Kwa upande wao viongozi wa Amani akiwemo zinduma kambwanga ambaye ni Mwenyekiti wa taasisi ya kina mama wa kiislamu Mkoani Tabora amewataka waumini wenzake wadumishe Amani na umoja katika nchi 

"Tunapoona tukio kama hili ni vyema kuchukua tahadhari siyo kukimbilia eneo la tukio siyo la kwanza kutokea Mungu awatie nguvu wale wote waliofikwa na msiba "Amesema Zinduma

Hata hivyo katika suala hiyo waumini wa madhehebu mbalimbali Wametakiwa kumcha Mwenyezi Mungu na kutii Sheria za nchi kama vitabu vitakatifu vinavyofundisha Maadili Mema.
 Pichani ni Sheikh mkuu wa Mkoa wa Tabora Alhaj Ibrahimu Mavumbi Akiongea na waandishi wa habari.
 Pichani ni waumini wa dini ya kiislamu  mkoani Tabora wakiswali dua kuadhimisha sikukuu ya Eid Al Adha katika kiwanja cha Ally hassan Mwinyi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...