Mamia ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam hii leo Jumatano Agosti 14, wamejitokeza kwa wingi ili kuungana na Benki ya Exim Tanzania ambayo kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS) waliendesha zoezi la uchangiaji damu kwa ajili kuwasaidia majeruhi wa ajali ya moto iliyosababishwa na lori la mafuta lililopinduka na kulipuka eneo la Msamvu Mkoani Morogoro ambapo watu zaidi ya 70 walifariki dunia na wengine kujeruhiwa.

Zoezi hilo litakalodumu kwa siku tatu mfululizo limefanyika kwenye viunga vya Stendi ya mabasi ya Mbagala jijini Dar es Salaam ambapo imeshuhudiwa idadi kubwa ya wakazi wa jiji hilo wakijitokeza kwa wingi ili kujitolea damu huku wadai kuwa muitikio huo umetokana na kuguswa kwao na tukio hilo la kusikitisha lililotokea mkoani Morogoro.

Meneja Masoko na Mahusiano ya jamii wa Benki ya Exim, Bw Abdulrahman Nkondo (alievaa kofia nyeupe) akiwagawia vinywaji baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwa wingi kwenye viunga vya Stendi ya mabasi ya Mbagala jijini Dar es Salaam ili kuchangia damu kwa ajili ya majeruhi wa ajali ya moto iliyosababishwa na lori la mafuta lililopinduka na kulipuka eneo la Msamvu Mkoani Morogoro ambapo watu zaidi ya 70 walifariki dunia na wengine kujeruhiwa. Zoezi hilo la siku tatu limeratibiwa na benki hiyo kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS)na linatarajiwa kukamilika Agosti 16.



Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam waliojitokeza kwenye viunga vya Stendi ya mabasi ya Mbagala jijini Dar es Salaam wakifuata taratibu ili kuchangia damu kwa ajili ya majeruhi wa ajali ya moto iliyosababishwa na lori la mafuta lililopinduka na kulipuka eneo la Msamvu Mkoani Morogoro ambapo watu zaidi ya 70 walifariki dunia na wengine kujeruhiwa. Zoezi hilo la siku tatu limeratibiwa na benki ya Exim Tanzania kwa kushirikiana na Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS)na linatarajiwa kukamilika Agosti 16.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...