Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas (kulia) akipokea taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Mtafungwa baada ya kuwasili Mkoni Morogoro baada ya kutokea ajali ya lori lililoungua moto na kusababisha vifo vya watu 62 na wengine 72 kujeruhiwa katika eneo la Msamvu Itigi Mkoani humo. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Maafa, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Nasser Mwakamboja.
Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas akikagua lori la mafuta lililopata ajali na kuungua moto Msamvu Itigi Mkoani Morogoro na kusababisha vifo vya watu 62 na wengine 72 kujeruhiwa. Nyuma yake ni Mkuu wa Kitengo cha Maafa, Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Nasser Mwakamboja
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, CGF Thobias Andengenye akizungumza na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas (katikati) na Mkuu wa Kitengo cha Maafa cha Jeshi la Polisi ACP Nasser Mwakamboja wakiwa katika hospitali ya Mkoa wa Morogoro walipowasili kuona majeruhi walioungua moto baada ya kutokea ajali ya lori lililoungua moto na kusababisha vifo vya watu 62 na wengine 72 kujeruhiwa katika eneo la Msamvu Itigi Mkoani humo. Picha na Jeshi la Polisi.

=========  ========  ========

*Wengine 70 wajeruhiwa, ni waliokuwa wanakuwanda kuzoa mafuta kwenye madumu 

*Wengi wao ni vijana wa bodaboda...mashahidi waeleza iliyokuwa eneo la tukio

Na Said MwisheheMichuzi TV

INASIKITISHA SANA! Ndivyo unavyoweza kuelezea kutokana  na kufariki dunia kwa watu 62 na wengine 70 kujeruhiwa na moto huo baada ya kulipukiwa kwa moto baada ya kukimbia  kutoa mafuta ya petroli baada ya gari aina ya roli kupinduka leo eneo la Msavu mkoani Morogoro.
 
Ajali hiyo imetolewa leo Agosti 10,2019 asubuhi katika eneo hilo la Msavu ambapo mashuhuda wa ajali hiyo wameiambia.Michuzi TV kuwa roli ya mafuta ilipinduka baada ya kumkwepa dereva bodaboda,hivyo roli likaacha njia.

Mmoja wa mashuhuda aliyejitambulisha kwa jina la  Bathromeo amesema baada ya ajali hiyo kutokea baadhi ya wananchi waliokuwa eneo hilo walianza kukimbia roli hilo wakiwa na madamu na ndoo wa ajili ya kubeba mafuta.

Hata hivyo baada ya roli kupinduka yaliyoanza kumwagika yalikuwa mafuta ya dizeli na nusu baadae yakaanza kutoka mafuta ya petroli."Ukweli mimi tangu ajali inatokea nilikuwa hapa na nimeona kila kilichokuwa kinaendelea.Wenzetu wenye tamaa waliamua kwenda na  madamu yao kuchukua mafuta,tuliwakataza lakini kwa tamaa zao waliamua kwenda.

"Hapa kuna mama alikuwa anauza chakula lakini baada ajali kutokea akachukua ndoo zake na kwenda kujaza mafuta na kisha kuyaweka hapa kwenye eneo analopikia.Matokeo yake yeye na mtoto wake wamekufa.Inasikitisha sana lakini ajali za aina hii zimekuwa zikitokea ila wananchi hatujifunzi,"amesema shuhuda huyo.


Kwa upande wake shuhuda mwingine amesema vijana waliokuwa eneo hilo yakiwemo wateja na waendesha bodaboda walionekana kubeba madamu na kwenda kuchota mafuta lakini ghafla ukasikika mlipuko mkubwa ambao tulisababisha gari hiyo kuanza kuwaka moto ambao ulikuwa unasambaa kwa kasi kubwa.

Hivyo kutokana na moto huo waliokuwa wakizoa mafuta wakaanza kuungua na wengi wamekuwa kwa kuteketea kwa moto huo ."Wamekufa watu wengi sana kwenye ajali hii ya kulipuka kwa roli la mafuta eneo hili la Msavu.

Amesema kuna baadhi yao walijaribu kukimbia lakini wakati huo tayari moto ulishakuwa umesambaa mwilini na kwamba kuna mmoja alijaribu kupanda juu ya moto lakini mti nao kuanza kuweka.

Hata hivyo tayari viongozi wa ngazi mbalimbali wa Mkoa wa Morogoro wamezungumzia ajali hiyo ambayo imesababisha vifo vya watu hao na kwamba wataendelea kutoa taarifa zaidi ya idadi ya rasmi ya waliopoteza maisha na waliojeruhiwa ingawa tayari watu 62 wameriporiwa kupoteza maisha na wengine zaidi ya 70 wamejeruhiwa kwa moto.

Wakati huo huo Kamanda mstaafu wa Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaaam Suleiman  Kova ambaye kwa sasa Mkurugenzi wa taasisi binafsi iliyosimamia maafa na majanga amesema ajali hiyo inasikitisha kwani idadi kubwa ya nguvu kazi imepotea.

Kova amesema kwa taarifa zilizopo hadi mchana huu tayari wameporipotiwa watu 62 wamepoteza maisha na wengine zaidi ya 70 wameungua na moto huo na sasa wakimbikizwa Hospitali ya Taifa Muhimbili ili kuokoa maisha yao.

"Ni ajali mbaya sana,watu wengi wamepoteza maisha.Ukweli wengi waliopoteza maisha ni wale waliokuwa wanakwenda kuchukua mafuta baada ya roli kupinduka. Ni mara nyingi elimu imekuwa ikitolewa kuhamasisha wananchi kutokimbilia mafuta baada ya gari kupinduka.

" Ni mara nyingi tumeshuhudia matukio ya aina hii na watu wamekuwa wakipoteza maisha.Ndio maana enzi zetu tuliamua kuanzisha Polisi shirikishi ili wananchi wenyewe kwa wenyewe wazuiane, Hata hivyo moto ni jambo la dharura,hivyo hakuna wa kulaumiwa na hata waliokufa hatuwezi kuwalaumu," amesema Kova.

Ametoa rai kwa wananchi kujiepusha  na  majanga kwa kuhakikisha wanachukua tahadhari na kusisitiza ajali hiyo ni mafunzo huku akitumia nafasi hiyo kutoa pole kwa Rais,Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  na Watanzania wote kwani msiba huo ni mkubwa.

Pia viongozi wa dini wamezungumzia ajali hiyo ambapo kwa sehemu kubwa wamesisitiza jamii.kujenga utamaduni wa kuchukua tahadhari na kubwa zaidi ni ajali inatopotokea cha kwanza ni kusaidia waliopata ajali badala ya kufanya tofauti na hivyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...