Anaandika Abdullatif Yunus - Michuzi TV

Timu ya Mpira wa Miguu ya Kagera Sugar FC inayocheza Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara imewasili salama Nyumbani Mkoani Kagera Baada ya Kucheza Mechi tatu za Ugenini,  na kuibuka na Ushindi mfululizo.

Timu hiyo imewasili Wilayani Missenyi ilipo kambi yao usiku, na Kisha kuelekea Bukoba Manispaa na kufanya mazoezi mepesi tayari kuziwinda pointi tatu muhimu dhidi ya mechi yao na wekundu wa msimbazi, klabu ya Simba ya Jijini Dar es salaam.

Mwalimu wa Timu hiyo ya wakata Miwa wa Kagera Mecky Maxime amesema kuwa Timu ipo katika hali mzuri na wako tayari kwa mapambano huku akiongeza kuwa Simba ni Timu kubwa hivyo maandalizi lazima yawe mazuri kuikabili akisistiza mashabiki kujitokeza kwa wingi kuipa nguvu Timu yao Iendeleze ushindi.


Kagera sugar inaingia tena kuwanjani Alhamisi hii kutafuta pointi tatu dhidi ya Simba huku rekodi zikionesha Timu hiyo kuifunga klabu ya Simba Mara tatu mfululizo kwa mechi waluzokutana, kubwa zaidi ni Timu ya Kagera imeanza msimu wa Ligi bila kufungwa na mechi zote ikiwa imecheza Ugenini, hivyo inaongoza Ligi kwa jumla ya Pointi tisa mpaka sasa.
Mwalimu wa Timu ya Kagera Mecky Maxime

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...