UTAMADUNI ni mfumo wa maisha ya watu jinsi wanavyoishi na maendeleo yao kijamii, kiuchumi, kisiasa na hivi ndivyo Tanzania inavyotunza utamaduni wake katika tamasha la utamaduni na Sanaa za jumuiya ya Afrika Mashariki linaloendelea kufanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar Es Salaam.

Mambo yanayofanya Tanzania kutunza utamaduni wake ni heshima iliyopo miongoni mwa jamii na husaidia watu kuwa na maendeleo kwa sababu ya heshima hiyo.

Tamasha la nne la JAMAFEST linaipamba Tanzania kwa kuwa nchi yenye utamaduni imara ndio maana Tamasha la utamaduni na Sanaa la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki linafanyika hapa nchini.

Tamasha hili la JAMAFEST linaunganisha nchi za Afrika Mahariki ili kila nchi ioneshe utamatuni wake kwa nchi mwanachama katika utamaduni na sanaa zake.

Tamasha la JAMAFEST ambalo hufanyika kila baada ya miaka miwili kuzunguka nchi wanachama ambalo hufanyika kwa muda wa siku nane huku likionesha kivutio vya nchi mbalimbali.


 Wasanii wakitumuiza katika Tamasha la Utamaduni na Sanaa la JAMAFEST linaloendelea kufanyika katika uwanja wa Taiafa jijini Dar es Salaam. Ikiwa Tanzania ni mwenyeji wa Tamasha hili.




 Kikundi cha Ngoma za asili hapa nchini ngoma ya unzinza kutoka Buchosa Sengerema jijini Mwanza wakitumbuiza katika tamasha la Jumuia ya Afrika Mashariki la JAMAFEST linaloendele kufanyika jijini Dar  es Salaam katika Uwanja wa Taifa. 
 Baadhi ya banda la utamaduni na sanaa katika maonesho ya Utamaduni na Sanaa kwa Nchi za jumuia ya Afrika Mashariki linalofanyika jijini Dar es Salaam Septema 21 hadi 28.
 Picha ya Kuchorwa.
 Kikundi cha Ngoma za asili kutoka Kukoba.


 Kikundi cha Ngoma ya asili kutoka Rwanda wakijiaanda kwa kutumbuiza.
 

 Kikundi cha Ngoma ya asili kutoka Mkoani Mbeya wakitumuiza katika tamasha la nchi za Juia ya Afrika Mshariki la Utamaduni na Sanaa la JAMAFEST linalofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


 Uremo uliotengenezwa na karatasi za kalenda katika banda la watu wa nchini Uganda. Hii ni katika Tamasha la Nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki la JAMAFEST linalofanyika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.



Mabanda ya kuonesha bidhaa za kiutamaduni na sanaa za nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki linalofanyika jijini Dar es Salaama katika uwanja wa Taifa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...