Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi Susan Mlawiakiwa katika picha ya pamoja na Vijana waliorejea kutoka nchini Kenyawalikokuwa katika mafunzo ya uandaaji wa filamu kwa mwaka mmojayaliyoandaliwa na Kampuni ya Multichoice chini ya dawati lijulikanalo kama“Multichioce Talent Factory Academy” baada ya kupokea taarifa ya mafunzowaliyopata walipomtembelea ofisini kwake Jijini Dodoma.
Meneja Biashara kutoka Kampuni ya Multichoice Bw.Jonson Mshana (kulia)
akitoa maelezo mafupi kuhusu “Multichioce Talent Factory Academy” iliyodhaminivijana wanne katika mafunzo ya uandaaji wa filamu kwa mwaka mmojayaliyoandaliwa na Kampuni hiyo Nchini Kenya walipofika ofisi ya Katibu MkuuWizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi. Susan Mlawi (kulia) kuelezeanamna walivyonufaika na mafunzo hayo.
Jamal Mohamed Kishuli ambaye ni miongoni mwa Vijana wanne
waliorejea kutoka nchini Kenya walikokuwa katika mafunzo ya uandaaji wa filamukwa mwaka mmoja yaliyoandaliwa na Kampuni ya Multichoice chini ya dawatilijulikanalo kama “Multichioce Talent Factory Academy” akizumngumza wakatiwalipomtembelea Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo BibiSusan Mlawi ofisini kwake Jijini Dodoma.
Bw.Wilson Nkya miongoni mwa Vijana wanne waliorejea kutoka nchini Kenyawalikokuwa katika mafunzo ya uandaaji wa filamu kwa mwaka mmojayaliyoandaliwa na Kampuni ya Multichoice chini ya dawati lijulikanalo kama“Multichioce Talent Factory Academy” akizumngumza wakati walipomtembeleaKatibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi Susan Mlawi(hayupo katika picha) ofisini kwake Jijini Dodoma.
******************

Na Shamimu Nyaki – WHUSM

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bibi.Susan Mlawiamewapongeza vijana wanne waliofanya vizuri katika mafunzo ya uaandaaji waFilamu yalioandaliwa na Kampuni ya Multichoice yaliyofanyika nchini Kenyaambapo amewataka kutumia taaluma waliyopata kutengeneza filamu bora zenyemaudhui ya kuitangaza nchi yetu na kuleta ushindani katika soko.

Katibu Mkuu Bibi. Susan ameyasema hayo leo ofisini kwake Jijini Dodoma baada yakutembelewa na vijana hao ambao amewataka kufika katika Bodi ya FilamuTanzania kuwasilisha uelewa waliopata na kushauri namna ambavyo Bodi hiyoinaweza kuwatumia katika tasnia hiyo.

“Nawapongeza sana kwa kufanya vizuri katika mafunzo mliopewa,naamini
mtayatumia vizuri katika kukuza vipaji vyenu na kusaidia mawazo kwa wengineambao hawajapata nafasi hii,Lakini pia mtatumia ujuzi na taaluma mliyopatakatika kuleta mapinduzi ya utengenezaji wa filamu hapa nchini”alisema Bibi Susan.

Naye Meneja wa masuala ya Biashara wa Kampuni ya Multichoice Bw.JonsonMshana amesema kuwa Kampuni hiyo imeanzisha dawati la kusaka vipaji vyauandaaji wa kazi za filamu (Multichoice talent Factory Academy) kwa Bara laAfrika ili vijana wenye uwezo na vipaji kupata fursa ya kuongezewa maarifapamoja na kutafuta ajira kwa njia rahisi.

Bw.Jonson ameongeza kuwa Kampuni hiyo kila mwaka inatafuta vijana wanneambao wanapatikana kwa kuomba nafasi hiyo na hatimaye kufanyiwa usaili nakujiunga na wenzao kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika ikiwemo Kenya,Ethiopia,Uganda na Nigeria.

Naye Kijana Jamal Mohamed Kishuli ambaye amejifunza “Art Designer” amesemakuwa vijana wanapaswa kujiamini katika kila wanachokifanya na kutokata tamaalakini pia zinapotokea fursa za kuonyesha uwezo wao basi wasisite kujitokeza ilikupata nafasi ya kujitangaza kupitia vipaji walivyonayo.

Vijana hao walikua katika mafunzo ya Uandishi wa Mswada (Script Writer),
Uandaaji (producer) Uongozaji (Directing) na Art Desgner ambayo wamejifunzakwa mwaka mmoja katika Chuo Kikuu cha Kenyata nchini Kenya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...