Na Jusline Marco-Arusha

Waziri wa habari, utamaduni sanaa na michezo Mhe. Harrison Mwakyembe amelitaka baraza la kiswahili Tanzania na baraza la kswahili Zanzibar kukaa pamoja na kuondoa tofauti ya lugha ya kiswahili iliyopo katika pande zote mbili na kuifanya kuwa na maana moja.

Mhe. Mwakyembe ameyasema hayo wakati akifungua Tamasha la Kimataifa la Kiswahili na Utamaduni katika chuo cha MS-TCDC Usa river Wilayani Arumeru Mkoani Arusha nwakutanisha wataalamu na wadau wa lugha ya kiswahili kutoja Zanzibar na Tanzania bara.

Aidha Waziri Mwakyembe amesema lugha ya kiswahili inaweza kutumika katika sekta zote na kuondoa zana potofu iliyopo kwa sasa ya kugeuza lugha hiyo kama sehemu ya masomo kwa wanafunzi na kuipa nafasi kubwa lugha ya kingereza hivyo ni vyema wanafunzi wakafundishwa lugha zote kwani wakizifahamu lugha zote mbili kwa Kiingereza na kiswahili wanaweza kufaulu vizuri katika masomo yao.

Naye katibu mtendaji baraza la kiswahili Zanzibar Mwanahija Juma amesema tofauti ya misamiati katika pande zote mbili zipo kutokana na usanifishaji wa baadhi ya maneno kuwa ya kiutamaduni.

Kwa upande wake Afisa utamaduni wa halmashauri ya Meru Senyaeli Pallangyo amesema kuwa jamii yoyote isiyokuwa na lugha yao utamaduni haupo hivyo lugha ya kiswahili inatumika kama kielelezo cha utaifa kwa Tanzania na nchi za Afrika Mashariki na Kati kwani ndiyo lugha inayowaonganisha watanzania ili kuondoa ukabila kwasababu karibu asilimia 90 ya watanzania huzungumza kiswahili.

Hata hivyo Tamasha hilo linafanyika kwa mara ya kwanza Nchini Tanzania tangu kusitishwa mnamo mwaka 2007 na linatarajiwa kuhitimishwa kesho huku kauli mbiu ikiwa ni Tukienzi Kiswahili na Utamaduni kama nyenzo muhimu za maendeleo.
 Waziri wa habari,utamaduni,sanaa na michezo Mhe.Harrison Mwakyembe akizungumza jambo na mwalimu wa lugha ya kiswahili katika chuo cha MS-TCDC Joachim Aloyce Kisanji katika Maadhimisho ya Tamasha la  Kimataifa la Kiswahili na Utamaduni lililifanyika Wilayani Arumeru Mkoani Arusha.
 Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Harrison Mwakyembe akitoa nasaha zake mbele ya wataalamu na wadau wa lugha ya kiswahili waliohudhuria katika Tamasha hilo
Baadhi ya wadau wa lugha ya kiswahili wakiguatilia ujumbe unaotolewa na waziri wa habari,utamaduni,sanaa na michezo Harrison Mwakyembe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...