NA K-VIS BLOG/Khalfan Said-TABORA
MKUU wa Mkoa wa Tabora Mhe. Aggrey Mwanry amewalinganisha walimu na silaha aina ya Katyusha iliyotumiwa na majeshi ya Muungano wa Kisovyeti (Soviet Union) au Urusi wakati wa vita Kuu ya Pili ya Dunia kwa vile huwa hawashindwi katika jambo lolote.
Mhe. Mwanry ameyasema hayo leo Septemba 16, 2019 Mkoani Tabora wakati akifungua Kongamano la Walimu la “Amsha Amsha na Mwalimu Bank”  lililoandaliwa na Mwalimu Commercial Bank kwa lengo la kutoa elimu ya fedha ikiwa ni pamoja na kujenga hamasa kwa walimu kutumia huduma za benki hiyo ambayo kwa kiasi kikubwa inamilikiwa na walimu nchini.
“Katyusha ni silaha iliyotumiwa na majeshi ya Muungano wa Kisovyeti (Soviet Union) au Urusi kwenye vita Kuu ya Pili ya Dunia,  na iliwapatia mafanikio makubwa katika mapambano hayo, na mimi walimu wangu Mkoani Tabora huwa nawalinganisha na silaha ya Katyusha kwani huwa hawashindwi kitu, wamenisaidia sana katika kampeni mbalimbali za maendeleo hapa Tabora ikiwemo ile ya upandaji miti ambayo imefanikiwa.” Alisema.
Alisema kwa niaba ya serikali Mkoani Tabora na wananchi wa Mkoa wa Tabora na Walimu kwa ujumla wako tayari wanaikaribisha benki ya Biashara ya Mwalimu mkoani humo ikiwa ni pamoja na kutumia huduma zake.
“Wameona isiwe tu kazi ya kufundisha darasani bali wameona wanasweza kutengeneza kitu kinachoitwa Benki ya biashara ya Mwalimu, umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu, ukienda benki wao hawaangalii hivi mnavyofikiria wanaangalia umeingiza kiasi gani na utachukua kiasi gani na umekopa shilingi ngapi na utarudisha kiasi gani nawapongeza kwa kuwa na chombo hiki.” Alisema.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank, Bw. Richard Makungwa alisema, moja ya mikakati ya benki hiyo kwa sasa ni kuhakikisha inawafikmia walimu nchi nzima na wameanza kwa kongamano kama hilo mkoani Kigoma kwa nia ya kutoa elimu ya fedha lakini pia kujenga hamasa kwa walimu kutumia huduma za benmi hiyo ambayo inamilikiwa na walimu kwa kiasi kikubwa.
“Benki yetu sasa ina miaka mitatu tangu ianze shughuli zake, benki hii ni mali yenu, tumieni huduma za benki yenu, tayari tuna matawi mawili Dar es Salaam, na tumefungua ofisi kwenye mikoa ya Morogoro, Mwanza na Mbeya na tunakusudia kufanya hivyo kadri muda unavyokwenda na ndio maana tuko hapa leo kuamsha amsha mwalimu na benki yenu.” Alifafanua Bw. Makungwa ambaye alifuatana na Kaimu Mkuu wa Biashara na Masoko, Bi. Leticia Ndongole na Mkurugenzi wa Fedha Bw. Selemani Kijori.
Aidha washiriki nao wamepongeza hatua ya uongozi wa benki kuwafikia huko mikoani na kushauri kuwa benki lazima iwe karibu na wateja wake ili kujenga kuaminiana.
 Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanry, akifungua kongamano la walimu la "Amsha Amsha na Mwalimu Bank" Mkoani humo kwenye ukumbi wa Chama cha Walimu Septemba 16, 2019. Kongamano hilo lililoandaliwa na Mwalimu Bank, lililenga kutoa elimu ya fedha kwa walimu ikiwa ni pamoja na kutoa hamasa kwa walimu kuitumia benki hiyo ambayo asilimia kubwa ya wanahisa wake ni walimu.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc, Bw. Richard Makungwa.(kulia), akitoa hotuba yake kwenye kongamano hilo. Katikati ni Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanry na Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Mkoa wa Tabora, Bw.Norbert Pandisha.
  Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanry, akifungua kongamano la walimu la "Amsha Amsha na Mwalimu Bank" Mkoani humo kwenye ukumbi wa Chama cha Walimu Septemba 16, 2019. Kulia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc, Bw. Richard Makungwa.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc, Bw. Richard Makungwa.(kulia), akitoa hotuba yake kwenye kongamano hilo. 
  Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc, Bw. Richard Makungwa.(kulia), akitoa hotuba yake kwenye kongamano hilo. 
  Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc, Bw. Richard Makungwa.(kulia), akitoa hotuba yake kwenye kongamano hilo. 
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanry (kulia) na Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Mmoani Tabora (WCT), Bw. Norbert Pandisha, wakimsikiliza Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bw.Aron Masalu, (kushoto), wakati akitoa hotuba yake kwenye kongamano hilo. 
 Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Mmoani Tabora (WCT), Bw. Norbert Pandisha
 Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Bw.Aron Masalu
 Baadhi ya walimu wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Aggrey Mwanry (hayupo pichani).
 Kaimu Mkuu wa Biashara na Masoko Mwalimu Commercial Bank Plc. Bi. Leticia Ndongole akitoa elimu ya fedha kwa washiriki.
 Mshiriki akizungumza kwenye kongamano hilo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc. Bw. Richard Makungwa (kulia), akiwa na Kaimu Mkuu wa Biashara na Masoko wa benki hiyo. Bi. Leticia Ndongole wakisikiliza maoni ya washiriki.

 Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Mwalimu Commercial Bank Plc. Bw. Richard Makungwa (katikati), akijadiliana jambo na Kaimu Mkuu wa Biashara na Masoko wa enki hiyo na Afisa Uhusiano, Bw. Said Rajabu wakati wa kongamano hilo.
  Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.
 Washiriki wakiwa kwenye kongamano hilo.


 Baadhi ya washiriki wakisikiliza hotuba ya Mkuu wa Mkoa.
 Mwenyekiti wa Chama cha Walimu Mkoa wa Tabora, Bw.Norbert Pandisha, (wapili kulia), Katibu wa CWT Mkoa wa Tabora, Bw.Aron Masalu (watatu kulia), Mkurugenzi wa Fedha wa MCB, Bw.Selemani Kijori (kushoto) na Kaimu Mkuu wa Biashara na Masoko, Bi. Leticia Ndongole.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Mhe. Aggrey Mwanry (kulia), akifurahia jambo na Afisa Uhusiano wa benki hiyo, Bw. Michael Kachala

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...