Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Watu wenye Ulemavu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Filbert Kawemwamwa. wa akieleza umuhimu wa ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara wakati wa kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019, kushoto kwake ni Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge), Parkshard Mkongwa.
Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Waziri Mkuu na Bunge), Parkshard Mkongwa akieleza umuhimu wa ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara wakati wa kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019, kulia kwake ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Watu wenye Ulemavu wa Ofisi hiyo, Filbert Kawemwamwa.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, wakati wa kujadili namna ya ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019.
Mwenyekiti wa SHIVYAWATA, Ummy Ndeliyanaga, akieleza umuhimu wa ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara wakati wa kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019.
Mkurugenzi wa Programu, Shirika la Kimataifa la ADD, Rose Tesha, akieleza umuhimu wa utetezi wa pamoja wa masula ya watu wenye ulemavu wakati wa kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, wakati wa kujadili namna ya ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019.
Mkalimani kwa kutumia lugha ya alama, Edna James, akieleza umuhimu wa utetezi wa pamoja wa masula ya watu wenye ulemavu wakati wa kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu wakimsikiliza Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Watu wenye Ulemavu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Filbert Kawemwamwa. wakati wa kikao cha Menejimenti ya wizara hiyo na , viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, wakati wa kujadili namna ya ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019.

………………….


Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) imewahakikishia watu wenye ulemavu nchini kupitia Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) kuwa itaendelea kujumuisha masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti kwa ngazi ya Wizara ili kuweza kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata huduma bora na stahiki.

Akiongea wakati wa kikao kazi kuhusu ushawishi na utetezi pamoja na ujumuishwaji wa masuala ya watu wenye ulemavu katika mipango na bajeti ngazi ya wizara, kilicho washirikisha Menejimenti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, viongozi kutoka SHIVYAWATA na Shirika la Kimataifa la ADD, leo jijini Dodoma, tarehe 16 Septemba, 2019, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Watu wenye Ulemavu wa Ofisi hiyo, Filbert Kawemwamwa amebainisha kuwa lengo la kikao hicho ni kuibua mikakati ya ujumuishaji, usimamizi na utekelezaji wa masuala watu wenye ulemavu nchini.

“Katika kuhakikisha kuwa mipango na bajeti ngazi ya wizara zinajumuisha masuala ya watu wenye ulemavu tutaendelea kukutana na wizara nyingine saba za kisekta ili kuweza kuhakikisha mipango ya maendeleo yao inaweza kuwafikia watu wenye ulemavu hasa walio vijijini, kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Maendeleo na Huduma ya Watu wenye Ulemavu ya Mwaka 20014” amesistiza Kawemwamwa

Awali akiongea katika kikao hicho Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA), Ummy Ndeliyanaga, ameshukuru kwa jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya Tano, inayoongozwa na Dkt. John Pombe Magufuli katika kuboresha huduma za msingi za watu wenye Ulemavu nchini, hata hivyo amebainisha kuwa wanazo hoja za msukumo kumi ambazo anaamini utekelezaji wake ukikamilika zitaboresha huduma na maendeleo kwa watu wenye ulemavu nchini.

“Tayari serikali kupitia ofisi ya Waziri Mkuu imeshaunda madawati ya watu wenye ulemavu katika wizara na taasisi zake tunaomba majukumu ya maofisa hao yapitiwe upya, pia uanzishwaji wa mchakato wa uundwaji wa mfuko wa Kitaifa wa watu wenye Ulemavu, masuala mengine ni kuanzishwa kwa rejista ya watu wenye ulemavu, kupitia sheria ya watu wenye ulemavu, Makakati wa ufukiwaji wa 3% ya watu wenye ulemavu kwenye kila taasisi inayo ajiri watu kuanzia 20” amesema Ndeliyanaga

Ameongeza kuwa wanaomba serikali isisimamie ukamilishwaji wa mchakato wa uandaaji wa taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa umoja wa mataifa wa haki za watu wenye Ulemavu, pamoja na kuwaelekeza waajiri wote kuandaa na kuwasilisha taarifa ya mwaka ya hali ya ajira kwa watu wenye ulemavu katika taasisi zao, pia ukamilshawaji wa mwongozo wa viwango vya ufikikaji wa miundo mbinu, Mipango ya Kisekta pamoja na Baraza la ushauri la watu wenye ulemavu kuhakikisha linafanya kazi kikamilifu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Programu, Shirika la Kimataifa la ADD, Rose Tesha, amefafanua kuwa shirika hilo limeamua kuunga juhudi za serikali za kuwahudumua watu wenye Ulemavu kwa kuwezesha SHIVYAWATA kukutana na wizara za kisekta ili kuweza kuhakikisha kuwa wanaweza kuzitetea vizuri fursa na haki za watu wenye ulemavu hapa nchini.

Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) iliundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Tangazo kwenye gazeti la Serikali Na.144 la mwezi Aprili, 2016. Pamoja na majukumu mengine Ofisi hiyo inajukumu la kusimamia utekelezaji wa sera, sheria, AMiongozo, Kanuni na Viwango vya Ubora katika utoaji wa huduma za watu wenye ulemavu nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...