Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Mchezo Dkt. Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi habari kuhusiana na Tamasha la Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki (Jumafest) litalifanyika Tanzania katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii 
WAZIRI wa habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Herrison Mwakyembe ameutaka Umma wa watanzania kujitokeza  kwa  kushiriki kwenye tamasha   la kimataifa la utamaduni wa Afrika mashariki (Jamafest) linalotegemea kufanyika katika Uwanja wa taifa jijini Dar es salaam Septemba 21 hadi 28 mwaka huu.

Dkt. Mwakyembe ameyasema hayo wakati wa mkutano wa Waandishi Habari kuhusiana  tamasha hilo amesema matarijio ya nchi kuwa  yetu kama mwenyeji wa  tamasha ni pamoja kuvunja rekodi ya maonesho ya  kuonyesha vipaji tulivyonavyo, kazi  mbalimbali  za mtanzania ikiwemo kuhifadhi na kulinda utamaduni wa mtu mweusi kupitia tasnia ya sanaa itakayo leta taswira ya kiushindani.

"Watanzania wote hapa nchini wahudhurie  kwenye onesho kubwa la kitamaduni ambayo lengo letu ni kuonyesha roho ya Afrika ambyo ni utamaduni  katika nyanja mbalimbali za sanaa," amsema Dkt.Mwakyembe

Dkt.Mwakyembe amesema kuwa tamasha hilo litawashirikisha wasanii na wajasiriamali kutoka nchi sita za Jumuiya ya Afrika mashariki zikiwemo Kenya , Uganda , Burundi, Rwanda na Tanzania kwa kuonyesha tamaduni za nchi zao.

Tamasho hilo limeratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Wizara ya habari Utamaduni Sanaa na michezo kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali  wa tasnia ya sanaa ili kuweza kufanikisha hilo.

Kwenye maadhimisho hayo wasanii wetu nchini wakiongozwa na Peter Msechu wameandaa wimbo maalumu utakaobaba ujumbe wa utamaduni wetu kwa ajili ya kulipamba tamasha hilo.

Dkt. Mwakyembe amesema tamasha hilo la kimataifa litawashirikisha wachonga vinyago, wabunifu wa mavazi,wasuka mikeka, watengenezaji wa nywele, wanamuziki wa dansi , watunga riwaya na michezo ya kuigiza.
Tamasha hilo litazinduliwa na Septemba 22 na Mmoja wa kiongozi wa juu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...