BODI ya Utalii nchini imeendelea na jitihada zake za kuhakikisha sekta ya utalii inakua na kuchangia uchumi wa taifa ambapo sasa wanaenda kutekeleza mkakati wa kutumia muziki na filamu kwa kuwatumia watayarishaji na wacheza filamu kutoka kampuni maarufu ya kutengeneza filamu ya 3rd Rock Multimedia ya nchini India inayotengeneza filamu za Bollywood ambao watakuja nchini  kutengeneza video na filamu za wasanii wa India katika mazingira ya Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari wakati akiwapokea wageni hao mwenyekiti wa bodi ya utalii jaji Thomas Mihayo amesema kuwa wageni hao wamekuja kuangalia maeneo ya kupiga picha na kurekodi video ambayo watakuja kuyafanyia kazi mwezi Agosti mwaka huu na kueleza kuwa kampeni hiyo imelenga kuvuna watalii wengi katika soko la India ambalo ni miongoni mwa masoko muhimu sana nchini huku mikakati ya kuhakikisha watalii wengi zaidi wanazidi kumiminika nchini utazidi kusimamiwa.

Amesema kuwa ujio wa mtayarishaji wa filamu Raj Suri Harvinder Sigh na mmiliki na mwongozaji video kutoka kampuni ya 3rd Rock Multimedia Amandeep Sighn ni fursa kubwa hasa kwa kutangaza mandhari na vivutio vya Tanzania kupitia filamu za Boolywood, hivyo ni vyema wasanii wa Tanzania wakatumia vyema fursa hiyo katika kujitangaza.

Jaji Mihayo amesema kuwa mkakati huo utaendelea kuitangaza nchi na vivutio vilivyomo katika soko la India kwa kuonesha filamu na picha katika televisheni na mitandao yao ya kijamii itasaidia kutangaza utalii wa Tanzania.

Amandeep Sighn ameeleza kufurahishwa na mazingira ya Tanzania na kusema kuwa yanafaa katika kazi zao. Amesema kuwa mwezi Oktoba watakuja wasanii 40 kutoka India ambao watajumuisha wanamuziki na waigizaji ili waweze kupata kitu tofauti na kuutangazia ulimwengu vivutio vinavyopatikana Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...