Na Khadija Seif, Globu ya Jamii
RAIS wa Zanzibar, Dr. Mohammed Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la 'Utalii Kusini' lililoandaliwa na balozi wa hifadhi za utalii Nangasu Warema .

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Warema amesema Tamasha hilo linatarajiwa kufanyika septemba 20 hadi 22 mwaka huu.

Amesema lengo la Tamasha hilo ni kukuza utalii wa kusini na kuhamasisha wawekezaji  kujitokeza kwa wingi ili kuboresha mazingira ya vivutio vya nchi ya Tanzania.

"Lengo la tamasha hili kukuza utalii wa kusini  kama mikoa mingine inavyopewa thamani kutokana na vivutio vilivyopo," amesema Warema.

Kwa upande wake Miss wa Tanzania 2018, Queen Elizabeth Makune amesema watanzania wanapaswa kutangaza vivutio vya utalii ili kujitangaza zaidi katika nchi za kigeni.

"Mkoa wa Kusini  umekuwa na vivutio mbalimbali vya kuwavutia watalii,
ifike mahali watanzania watangaze utalii  kwa manufaa ya nchi yetu,"
amesema Queen Elizabeth.

Msanii wa filamu za bongo nchini, Rose Ndauka amemalizia kwa kuwashauri wasanii kutangaza utalii wa nchi yao kupitia kazi wanazozifanya kwa lengo la kuongeza kipato katika sekta ya utali

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...