Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akipokea taarifa kutoka kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Hudson Kamoga wakati wa ziara yake ya kikazi Wilayani humo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akizungumza wakati akikagua ujenzi wa Hospital ya Wilaya ya Mbulu inayoendelea kujengwa Wilayani hapo
Muonekano wa baadhi ya majengo ya Hispital ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu yanayoendelea kujengwa Wilayani hapoWaziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo akiagana na viongozi wa Halmashauri ya Mbulu wakati wa ziara yake Wilayani humo.

………………….

Nteghenjwa Hosseah, Dongobesh

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amepongeza Uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu kwa usimamizi makini wa ujenzi wa Hospital ya Wilaya inayoendelea kujengwa katika kata ya Dongobesh.

Waziri Jafo ametoa pongezi hizo baada ya kutembelea eneo linapojengwa Hospital ya Wilaya na kuridhishwa na hatua iliyofikiwa katika ujenzi huo ukiacholia mbali changamoto walizokutana nazo wakati wa ujenzi.

Hakina Mbulu nimewaelewa Hospital ya Wilaya inavutia mmejenga majengo mazuri yenye ubora unaotakiwa na mmezingatia maagizo tuliyotoa katoka ujenzi wa hospital hizi za Wilaya

Mmenifurahisha ingawa majengo yenu hayajakamilika lakini nimeziskia changamoto mzilokutana nazo na namna mlivyokabiliana nazo kwa sababu hazikua kikwazo cha kukwamisha kazi hii mmeweza kuzitatua na ujenzi ukaendelea kama kawaida.

“Mbulu mmewapita hata Halmashauri zingine ambazo hawakuwa na changamoto zozote nyie mmekabiliana na changamoto za kutosha lakini bado kazi yenu imekua nzuri na inayopendeza hongereni sana na muendelee na kazi hii nzuri kwenye miradi mingine” Alisema Jafo.

Pia Waziri Jafo amempongeza Mbunge wa Halmashauri ya Mbulu Mhe. Flatei Massay kwa jitihada zake anazozifanya za kutetea wananchi na kuhakikisha wanapata miradi ya maendeleo.

Mbunge wenu anawapenda sana watu wa Mbulu anapambana kuhakikisha miradi mingi ya maendeleo inawafikia wananchi wake na kuleta maendeleo katika Jimbo la Mbulu Vijijini alisema Jafo.

Msidhani kuwa miradi hii imekuja kwenu kwa bahati tu kuna jitihda kubwa zimefanyika mpaka mkapata fedha za ujenzi wa Jengo la Halmashauri , mkajengewa kituo cha Afya Dongobesh na zadi mkapata tena Tsh Bil 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospital za Wilaya hii ni miradi mingi sana kwa Halmashauri moja kuipata katika kipindi chwa mwaka mmoja wa fedha.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbuli Mhe. Chelestino Mofugo amesema pamoja na changamoto walizokutana nazo wakati wa ujenzi, Wananchi wa Dongobesh wametoa ushirikiano wa kutosha wakati wote wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

“Mhe. Waziri Jafo napenda ufahamu kuwa wananchi wa Dongobesh ndio waliotupa hili eneo bure kabisa kwa ajili ya ujenzi wa Hospital ya Wilayah ii inaonyesha utayari wa hali ya juu ya wananchi hawa kuipokea Halmashauri ya Wilaya kuhamia katika eneo hili na hili limetusaidia sana katika kufanikisha ujenzi wa hospital yetu hii unayoiona” alisema Mhe. Mofugo.

Akisoma Taarifa ya ujenzi wa Hospital ya Wilaya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mbulu Hudson Kamoga alisema changamoto kubwa liyokutana nayo wakati wa kuanza ujenzi ni pamoja ni miamba migumo ya eneo la hospital pamoja na kuwa na maeneo oevu ambayo kwa kiasi kikubwa yalirudisha nyumba kasi ya ujenzi.

“Hii changamoto ya kukutana na mwamba mgumu ilitulazimu kutafuta milipuko na wataalam wa kuilipua ili kutoa huo mwamba lakini tulijitahidi kadiri ya uwezo wetu kulifanyia kazi kwa haraka na kufanikiwa kuondoa mwamba huo kisha ujenzi ukaendelea” alisema Kamoga.

Pia Kamoga aliotoa ombi maalumu kwa Waziri Jafo kuwa wanaomba kupatiwa Mhandisi wa Halmashauri au mafunzi mchundo ili awasaidie katika kusimamia miradi ya ujenzi kwa kuwa aliyepo sasa anazidiwa na kazi na endapo inatokea anapata dharura kazi zote za ujenzi zinasimama kwa muda kusubiri amalize dharura yake ili ahakiki ubora wa kazi.

Ujenzi wa hospital ya Wilaya ya Mbulu umefikia asilimia 80 na ni moja wapo ya hospital za Wilaya 67 zinazoendelea kujengwa Nchi Nzima.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...