Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji (wa
tatu kushoto), akikabidhi tuzo ya mshindi wa tatu katika kitengo cha
makampuni bora ya mwaka katika eneo la uwekezaji katika sekta za
kibenki kwa Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria wa Benki ya Biashara ya
DCB, Regina Mduma wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa wanachama wa DSE
jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Wengine pichani kutoka kushoto ni;
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Soko la Hisa la Dar es salaam, Moremi Marwa,
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko na Mitaji na Dhamana (CMSA),
Nicodemus Mkama na Ofisa katika kitengo cha Sheria wa DCB, Grace Ringo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji (kulia), akishikana
mikono Mkurugenzi wa Kitengo Cha Sheria was Benki ya DCB, Regina Mduma,
baada ya kumkabidhi iliyoshinda benki hiyo ya mshindi wa tatu katika
kitengo cha makampuni bora ya mwaka katika eneo la uwekezaji katika
sekta za kibenki wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa wanachama wa DSE
jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kushoto ni Ofisa katika kitengo cha
Sheria wa DCB, Grace Ringo.
Mkurugenzi katika Kitengo cha Sheria wa Benki ya DCB,
Regina Mduma (kulia), na Ofisa wa Kitengo hicho Grace Ringo wakionesha
tuzo hiyo mara baada ya kukabidhiwa na Naibu Waziri wa Fedha
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...