Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya DCB,Godfrey Ndalahwa akizungumza mbele ya Waandishi wa habari na Wageni waalikwa mbalimbali (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa akaunti maalum ya akiba ya mpango wa elimu ijulikanayo kwa jina la DCB Skonga,leo jijini Dar.Kulia ni Mkurugenzi wa Biashara ,James Ngaluko na kushoto ni Balozi wa benki hiyo kupitia akaunti ya DCB Skonga,Zamaradi Mketema.
Kulia ni Mkurugenzi wa Biashara wa Benki ya DCB,James Ngaluko akitoa ufafanuzi zaidi kuhusu akaunti ya DCB Skonga,amesema kuwa kupitia bidhaa ya DCB Skonga mteja anaweza kuchagua mpango wa aina mbalimbali wa kuweka akiba pamoja na muda wa uwekezaji kulingana na umri,gharama na muda wa masomo ya mtoto wake, "hiyo ndiyo njia salama ya kuweka akiba yako huku ukihakikishiwa elimu ya mtoto wako na mwisho wa muda uliochagua (mwaka 1 hadi 17) benki itakupa akiba yako yote ambayo pia itakusaidia kutimiza malengo yako mengine mbalimbali ya kimaisha",alisema Ngaluko.
Balozi wa benki ya DCB kupitia bidhaa ya DCB Skonga,Zamaradi Mketema akieleza namna gani akaunti hiyo inavyoweza kuisaidia jamii katika maeneo mbalimbali,amefafanua pia kuwa akaunti hiyo haijakaa kibiashara,imekaa katika mtindo wa kumsaidia mtu kuzifanikisha ndoto zake za kimaeendeleo ikiwemo elimu katika familia. "kwa hiyo akaunti hii imekuja kwa wakati muafaka kabisa,imekuja kutuokoa na kutuhakikishia kwamba hata jambo lolote likitokea ntaitumia akaunti hiyo kuhakikisha mtoto wangu anamaliza elimu yake bila tatizo lolote",alisema na kuongeza kuwa kupitia akaunti hiyo mtu anaweza kupata mkopo mpaka asilimia 50
Baadhi wageni waalikwa wakiwemo wafanyakazi wa beki ya DCB wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo wakati wa uzinduzi wa akaunti maalum ya akiba ya mpango wa elimu ijulikanayo kwa jina la DCB Skonga,leo jijini Dar.
Benki
ya Biashara ya DCB leo imezindua akaunti maalum ya akiba ya Mpango wa
elimu ijulikanayo DCB Skonga,ikilenga kumhakikishia mteja akiba na
uhakika wa elimu ya mtoto wake hadi chuo Kikuu.
Akizungumza katika uzinduzi wa akaunti hiyo leo jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki ya DCB,Godfrey Ndalahwa amesema kuwa DCB Skonga ni
akaunti maalum ya akiba inayo mpa mteja fursa ya kuweka akiba kila mwezi
ili kutimiza malengo aliyo jiwekea huku mteja akihakikishiwa elimu ya
mtoto wake hadi chuo kikuu
Ndalahawa
amesema benki ya DCB inaamini katika kutoa fursa zenye tija kwa wateja
wao na Watanzania kwa ujumla,kwa kuwaletea bidhaa nzuri zinazowapa tija
na faida lukuki."Kwa mara nyingine tena leo DCB inaandika historia
nyingine kwa kuzindua bidhaa mpya ya mpano wa elimu ijulikanayo DCB
SKONGA AKAUNTI,",alisema Ndalahwa.
Kwa upande wake Mkurugenzi
wa Biashara wa Benki ya DCB,James Ngaluko alisema kwa kupitia bidhaa
hiyo ya DCB Skonga mteja anaweza kuchagua mpango wa aina mbalimbali wa
kuweka akiba pamoja na muda wa uwekezaji kulingana na umri,gharama na
muda wa masomo ya mtoto wake.
"Hii
ni njia salama ya kuweka akiba yako huku ukihakikishiwa elimu ya mtoto
wako na mwisho wa muda ulio chagua (mwaka mmoja hadi 17 ) benki itakupa
akiba yako yote ambayo itakusaidia kutimiza malengo yako mengine
mbalimbali ya kimaisha",alisema Ngaluko.
Alisema
kuwa akaunti hiyo inampa fursa mteja kuchagua muda wa kuweka akiba
kutoka mwaka 1 hadi 17 na endapo atapoteza maisha au kupata ulemavu wa
kudumu kabla ya muda kuisha,tegemezi wake watarudishiwa kiasi cha fedha
alichowekeza kuanzia mwanzo wa mpango na vile vile mtoto atalipwa
gharama zote za elimu pamoja na hela ya matumizi ya shule kwa kipindi
chote kilichosalia cha mkataba.
Aidha
Balozi
wa benki ya DCB kupitia bidhaa ya DCB Skonga,Zamaradi Mketema amesema
akaunti hiyo ina umuhimu mkubwa kwa jamii,kwani inaweza kumsaidia mtu
katika maeneo mbalimbali katika kutatua changamoto zake ikiwemo sula la
elimu kwa familia yake.
"Akaunti hiio haijakaa kibiashara,imekaa
katika mtindo wa kumsaidia mtu kuzifanikisha ndoto zake za kimaeendeleo
ikiwemo elimu katika familia,kwa maana hiyo akaunti hii imekuja katika wakati
muafaka kabisa,imekuja kutuokoa na kutuhakikishia kwamba hata jambo
lolote likitokea ntaitumia akaunti hiyo kuhakikisha mtoto wangu
anamaliza elimu yake bila tatizo lolote",alisema Zamaradi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...