Na Karama Kenyunko, globu ya jamii.
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu
imemtaka mdhamini wa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu
ifikapo Novemba 21, mwaka huu kuleta mahakamani uthibitisho wa maendeleo
ya afya ya Lissu.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
imefikia hatua hiyo baada ya kesi ya uchochezi inayomkabili Lissu
kusimama kusikilizwa kwa takribani miaka miwili kwa sababu mshtakiwa
huyo anaumwa yuko Ubelgiji.
Mapema,
wakili wa Serikali, Estazia Wilson alidai mahakamani hapo kuwa, kesi
hiyo leo ilikuja kwa ajili ya usikilizwaji wa ushahidi wa shahidi wa
upande wa mashtaka lakini haiwezi kuendelea kwa sababu mshtakiwa Lissu
hayupo.
Mdhamini
wa mshtakiwa huyo, Robert Katula alidai Lissu bado anaumwa yuko nje ya
nchi.Kufuatia taarifa hiyo, hakimu Simba amemuamuru mdhamini tarehe
ijayo ya kesi afike na uthibitisho wa maendeleo ya mshtakiwa na kesi
imeahirishwa hadi Novemba 21 mwaka huu.
Mbali
na Lissu, washtakiwa wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni Mhariri wa
gazeti la Mawio, Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya
Jamana, Ismail Mehboob.
Lissu
na wenzake Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya
Jamana, Ismail Mehbooh wanakabiliwa na mashtaka matano ikiwamo la
kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka
2002.
Inadaiwa
kuwa Januari 12 hadi 14, 2016 katika jiji la Dar es Salaam, washtakiwa
watatu, Jabir, Mkina na Lissu, kwa pamoja waliandika na kuchapisha
taarifa za uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, ‘Machafuko yaja
Zanzibar’.
Katika
shtaka la pili wanadaiwa kuwa Januari 14, 2016 katika jiji la Dar es
Salaam, walichapisha habari hizo ili kuleta chuki kwa wananchi wa
Zanzibar.Mshtakiwa Mehboob anadaiwa kuwa Januari 13,2016 katika jengo la
Jamana lililopo Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam, alichapisha gazeti la
Mawio lililokua na taarifa za uchochezi.
Alidai mshtakiwa huyo pia alichapisha gazeti hilo bila ya kuwasilisha hati ya sheria ya kiapo kwa Msajili wa Magazeti.
Mbali
na mashtaka hayo washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kuwa Januari 14,
2016, Dar es Salaam, bila ya kuwa na mamlaka yoyote, waliwatisha na
kuwatia hofu wananchi wa Zanzibar wasiweze kuingia kwenye marudio ya
Uchaguzi Mkuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...