Timu ya madereva taxi watano kutoka Uingereza ilifanya ziara nchini kuanzia tarehe 28 Septemba hadi 10 Oktoba 2019. Ziara hiyo iliratibiwa na Wizara kupitia Ubalozi wetu London kwa kushirikiana na TTB. Timu hiyo ilikuja nchini kwa ajili ya kupanda mlima Kilimanjaro ikiwa ni zoezi la hisani ili kuchangisha fedha kwa ajili ya maveterani wa kijeshi (military veterans) huko Uingereza. 

Katika kutambua uamuzi mzuri wa timu hiyo kuuchagua mlima Kilimanjaro kwa zoezi hilo la hisani na kwa malengo ya kunufaika na ujio wao katika kutangaza vivutio vyetu vya utalii nchini Uingereza, Wizara ya Mambo ya Nje kwa kushirikiana na Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) iliwaandalia timu hiyo ziara ya kutembelea vivutio vya utalii mbalimbali hapa nchini zikiwemo mbuga za wanyama za Serengeti, Ngorongoro na Tarangire.

Vilevile, Timu hiyo ya madereva taxi baada ya kumaliza kutembelea vivutio vilivyotajwa hapo juu walitangazwa kuwa mabalozi wa hiari wa utalii (tourism goodwill ambassadors) wa Tanzania kwa lengo la kutangaza vivutio vya utalii vya hapa nchini wawapo katika shughuli zao huko Uingereza. Hafla ya kuwatangaza ilifanyika Hotel ya Mount Meru Arusha. Baada ya kutangazwa kuwa mabalozi wa hiari, walisaini Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya timu hiyo na TTB tayari kwa kutekeleza majukumu yao.

Tukio hilo lilihudhuliwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya maliasili na Utalii Dkt. Aloyce Nzuki, akimuwakilisha Mhe. Dkt. Hamisi Kigwangallah (Mb), Waziri wa Maliasili na Utalii na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo. Aidha, Mgeni Rasmi katika shughuli hiyo alikuwa Balozi wa Uingereza hapa nchini, Mhe. Sarah Cooke.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, 
Timu ya Madereva kutoka Uingereza ikipanda mlima Kilimanjaro kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya maveterani wa kijeshi (military veterans) huko Uingereza. 
Timu ya Madereva wa Taxi kutoka Uingereza ikiwa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro (Uhuru Peak). 

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Mrisho Gambo akitoa neno katika hafla ya uwekaji saini wa Hati ya Makubaliano (MoU) kati ya Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na Timu ya Madereva wa taxi watano kutoka Uingereza. Makubaliano hayo yalihusu timu ya madereva wa Uingereza kuwa Mabalozi wa hiari wa kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania nchini Uingereza. 
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Mhe. Sarah Cooke akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa TTB, Dkt. Devota Mdachi na Kiongozi wa Madereva wa Taxi wakiweka saini MoU. 
Hati ya Makubaliano baada ya kusainiwa ikioneshwa kwa wajumbe walioshiriki hafla ya uwekaji saini. 
Madereva wa Taxi, baadhi yao wakiwa na wenza wao baada ya hafla ya uwekezaji saini MoU 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...