Na Avila Kakingo, Globu ya Jamii.
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Pombe Magufuli atamani msanii mziki wa Kizazi kipya maarufu kama Bongo freva, Rajabu abdul a.k.a Hamonise anatamani agombee katika jimbo la Tandahimba lililopo mkoani Mtwara.
Ameyasema hayo leo Oktoba 15,2019 wakati wa ziara yake mkoani wa Lindi wakati akizungumza na wananchi wa wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi baada ya kumaliza kuhutubia.
"Na kumalizia nawapongeza sana waimbaji hawa wakinababa na mmoja alikuwa akisema sisi vijana na nilipo muona ni mzee kuliko mimi nikasema kumbe vijana wa hapa wanaumri mzuri, lakini nampongeza sana Hamoniza (Hamonise) sijui anatoka jimbo gani? anatoka jimbo gani huyu? Tandahimba!, Mbunge wa kule ni nani? Akhaaa nilitamani kweli Hamoniza aende akagombee kule akawe Mbunge wa Tandahimba ndugu zangu Asanteni Sana Mungu awabariki Sana". Amesema Rais Magufuli
Msanii Hamonise hivi karibuni aliondoka katika Kundi la WCB lilikuwa likisimamiwa na Msanii Nasibu Abdul maarufu kama Diamond na kuanza kujitegemea mwenyewe katika kazi zake za kimziki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...