Na Jusline Marco-Arusha.

Mbunge wa Arusha mjini,Godbless Lema ameahidi kutoa magari 20 yatakayogharimu milioni sita kwa ajili uhamasishaji wa uandikishaji wa daftari la wapiga kura.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amesema kuwa licha ya uhamasishaji kuwa mdogo pia mawakala wao hawapewi daftari ili kufahamu  tathimini ya waliojiandikisha kwa siku  ingawa wanayo haki ya kujua idadi hiyo ili kuondoa ubadhirifu wa majina yatakayoongezwa  kupitia mawakala wote.

"Tatizo la kuwanyima mawakala wetu  kujua idadi waliojiandikisha na uhamasishaji wa gari la matangazo kupita kwa kasi hivyo naomba wananchi wajitokeze kujiandikisha kwa wingi hili waweze kuchagua kiongozi atakayeleta maendeleo," alisema Mbunge huyo.

Aidha amesema pamoja na mawakala kutopewa ruhusa ya kukagua daftari hilo amewataka  wananchi kujitokeze kujiandikisha kwa wingi ili ifikapo Novemba mwaka huu wakafanye maamuzi sahihi ya kuchagua wenyeviti wa serikali za mtaa.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha demokrasia na maendeleo(Chadema) wa wilaya ya Arusha mjini,Innocent Kasanyage amesema kitendo cha mawakala wao kuzuiwa kujua idadi ya waliojiandikisha ni kinyume na sheria hivyo kama chama watapeleka malalamiko kwenye baraza la nidhamu msimamizi wa uchaguzi wa wilaya hiyo.

Akizungumza kwa njia ya simu Msimamizi wa uchaguzi jiji la Arusha,Mpena Bina amesema ni haki ya wakala wa uchaguzi kufahamu idadi ya watu waliojiandikisha kwa siku isipokuwa changamoto ni pale wakala anapochelewa kufika kituoni hukuta mwandikishaji akiendelea.

"Kwa kuwa changamoto hii nimeisikia kwako kwa Mara ya kwanza nitaifanyia kazi kama kuna baadhi ya watu wanawazuia mawakala kujua idadi ya waliojiandikisha," alisema Msimamizi huyo.
Mbunge waArusha Mjini Mhe.Godbless Lema akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mapema leo kuhusiana na baadhi ya mawakala wako walio katika vituo vya uchaguzi kuzuiwa kukagua daftari la uandikishwaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...