Ikiwa Imesalia siku moja kabla ya kufungwa kwa zoezi la kuandikisha wananchi kwenye Daftari la kudumu la Wapiga kura kwajili ya Kuchagua viongozi wa ngazi ya Mtaa, Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda kwa kutambua umuhimu wa zoezi hilo amewaelekeza wenye maduka kufungua maduka yao Kesho October 14 kuanzia saa tano ili kutoa nafasi kwa wananchi kwenda kujiandikisha.

RC Makonda amesema kwakuwa kesho ni Siku ya Kumbukumbu ya Miaka 20 ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ameona ni vyema Wananchi wote wakamuenzi Baba wa Taifa kwa kuhakikisha wanapata Nafasi ya Kutosha ya Kujiandikisha ili waweze kuchagua Viongozi wa mitaa wanaoweza kutatua matatizo yao.

Aidha RC Makonda amewasihi Wamachinga, Bodaboda, Makondakta, madereva, Viongozi wa Taasisi, wafanyakazi wa Bar, Saloon, wamiliki na wafanyakazi wa Sehemu za Starehe kuhakikisha wanajiandikisha kwenye Ofisi za Serikali ya Mtaa, Shule za Msingi,  sekondari na sehemu zilizowekwa mahema maalumu ya kujiandikisha.

EWE MWANANCHI TUMIA HAKI YAKO YA MSINGI YA KUJIANDIKISHA KWAAJILI YA KUCHAGUA VIONGOZI WENYE SIFA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...