Serikali imesema haitavumilia uzembe wa aina yeyote utakaofanywa na Wataalamu wa Ununuzi wa Ugavi katika kipindi hiki cha Uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuelekea mapinduzi ya Uchumi wa Viwanda.

Kauli hiyo imetolewa leo na  Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Michael John aliyemuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Filipo Mpango (Mb) wakati wa Mahafali 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam.

Michael John ametoa tahadhari kwa Bodi hiyo isipochukua hatua kwa uzembe wowote, Wizara ya Fedha itachukua hatua dhidi yao, amesema PSPTB inasismia sheria

"Katika hotuba yako umesema Bodi yako inaendelea kutoa miongozi na Maadili ya Kitaaluma, kusimamia mienendo na utendaji kwa Waalamu waliosajiliwa licha ya jitihada hizo bado taarifa mbalimbali za ukaguzi zinaonyesha kuwepo ununuzi holela usiozingatia utaalamu Bodi lazima iweke mikakati mipya  kukabiliana na jambo hilo,'' amesema Michael John

Hata hivyo, PSPTB imepongezwa kwa jitihada za utendaji ikiwa kuwafutia usajili na kuwafikisha mahakamani Wataalamu waliosabisha hasara kwa Taifa.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB), Godfred Mbanyi amesema Taasisi kumuajiri mtu asiyesajikiwa na Bodi hiyo ni kosa  la jinai na adhabu yake ni kifungo kisichozidi miaka miwili jela au faini ya milioni mbili au vyote kwa pamoja.

Kwa upande wake, Kamishna wa Idara ya Sera ya Ununuzi wa Umma kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Fredrick Mwakibinga amesema taaluma ya Ununuzi na Ugavi ipo kwenye majaribu kutokana na mienendo na tabia ambazo zipo kwenye Jamii kwa Wataalamu wake kutokana na kuhusiana na Fedha za Taasisi. 
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Michael John akizungumza kwenye mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo. Mkurugenzi huyo alimuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Filipo Mpango (Mb) kwenye mahafali hayo.
 Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi akizoma risala pamoja na kutoa neno kwa wahitumu wa Bodi hiyo wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
 Kamishna wa Sera ya Idara ya Ununuzi wa Umma kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Fredrick Mwakibinga akitoa nasaha  kwa wahitimu wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
 Mkurugenzi wa mafunzo wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Amani Ngonyani akisoma majina ya wahitimu wa Bodi hiyo waliofika kwenye mahafali ya 10 yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Afisa mwandamiza Masoko na mahusiano kwa Umma wa Bodi ya wataalamu wa ununuzi na Ugavi (PSPTB), Shamim Mdee(wa kwanza kulia) pamoja na wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Michael John akitoa zawadi kwa baadhi ya wanafunzi waliofanya vizuri kwenye mitihani ya Bodi wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Mwanasheria wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Suleiman Mnzava(kushoto) akiwalisha viapo vya maadili ya kazi waalamu wa Ununuzi na Ugavi walofika kwenye mahafali ya 10 ya Bodi  hiyo yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Wahitimu wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) wakila viapo vya kazi wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi  hiyo yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Wahitimu wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Michael John aliyemuwakilisha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Filipo Mpango (Mb) kwenye mahafali ya 10 ya Bodi  hiyo yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia mahafali ya 10 ya Bodi  hiyo yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.

Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi  akimuongoza mgeni rasmi Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Michael John kwa ajili ya kuongoza maandamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Michael John(katikati) akiongoza maandamano ya kitaaluma  ya mahafali ya 10 ya Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi mtendaji wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), Godfred Mbanyi  na kushoto ni Kamishna wa Idara ya Ununuzi wa Umma kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Dk. Fredrick Mwakibinga.
Wahitimu wa Bodi ya wataalumu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) wakifanya maadamano ya kitaaluma wakati wa mahafali ya 10 ya Bodi  hiyo yaliyofanyika katika viwanja vya Karemjee jijini Dar es Salaam leo.
Picha za pamoja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...