Na Eva Valerian na Ramadhani Kissimba, Washington DC

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango(Mb) amefanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa ‘Asian Infrustructure Investment Bank’ Bw. Danny Alexander jijini Washington DC. Katika mazungumzo na Benki hiyo wamekubaliana kusaidia katika miardi endelevu ya Miundombinu kama Barabara na Reli.

Mazungumzo hayo ambayo pia yalihudhuriwa na Waziri wa Fedha na Mipango wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Mhe.Mohammed Abdiwawa, Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga na Naibu Gavana wa Benki Kuu, Dkt.Yamungu Kayandabila yalikuwa na lengo la kuangalia fursa ambazo Tanzania inaweza kunufaika kutoka katika Benki hiyo.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe.Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) akiwa na Makamu wa Rais wa ‘Asian Infrastructure Investment Bank’ Katika mazungumzo yaliyofanyika kwenye ubalozi wa Tanzania Jijini Washington DC.

 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango(Mb) akiwa katika mazungumzo na Bw. Danny Alexander Makamu wa Rais wa ‘Asian Infrastructure Investment Bank’  yaliyofayika katika ukumbi wa mikutano wa Ubalozi wa Tanzania Jijini Washington DC. Kushoto kwa Mhe.Waziri ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Prof. Florens Luoga na Naibu Gavana, Dkt.Yamungu Kayandabila.
Makamu wa Rais wa ‘Asian Infrastructure Investment Bank’ akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt.Philip Isdor Mpango (Mb) kulia, na Waziri wa Fedha na Mipango Zanzibar, Mhe. Mohammed Abdiwawa. Kulia kwa Mhe. Mpango ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Mashimba Ndaki na kushoto kwa Mhe.Abdiwawa ni Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...